Na
Editha Karlo - Kigoma
CHAMA
cha waandishi wa habari wa Mkoa Kigoma(KGPC)imegawa vifaa mbalimbali vya
kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona kwa wanachama wake ili kuwasaidia
kufanya kazi zao kwa ufanisi katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa huo.
Vifaa
hivyo vimetolewa umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania(UTPC)kupitia
mpango wa utekelezaji wa mpango mkakati wa kuzisaidia club za waandishi wa
habari unaodhaminiwa na shirika la maendeleo la Sweden(SIDA).
Mratibu
wa Klabu hiyo Diana Rubanguka alisema kuwa kila mwanachama atapata
barakoa,glavu,chupa ya dawa ya kutakasa mikono(sanitaizer)ambavyo vitawasaidia
kujilinda na kujikinga na ugonjwa huo.
Diana
alisema vifaa hivyo vimetolewa umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania
(UTPC) kupitia mpango wa utekelezaji wa mpango mkakati wa kuzisaidia club za
waandishi wa habari unaodhaminiwa na shirika la maendeleo la Sweden (SIDA).
Rais
wa UTPC, Deogratias Nsokolo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa
habari wa Mkoa wa Kigoma alisema kuwa kutokana na hali ya mlipuko uliopo sasa
wa ugonjwa virusi vya corona walikubaliana na SIDA kutumia baadhi ya fedha
kununua vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo na kutoa mafunzo kwa wanachama juu
ya ugonjwa huo.
"Baadhi
ya mambo yaliyokuwa yafanyike mwaka huu yamehairishwa na fedha zilizokuwa
zimetengwa zimeelekezwa upatikanaji wa vifaa hivo kwaajili ya club zote za
Tanzania Bara na visiwani",alisema Nsokolo.
Alisema
kazi za waandishi wa habari zinahitaji kukutana na watu mbalimbali hivyo ni
muhimu kuwa na vifaa vya kujikinga na maambukizi hayo.
Nsokolo
aliwataka wanahabari wote nchini kuendelea kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya
ugonjwa huo kwa kuzingatia na kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa
afya na serikali ikiwa ni pamoja na kutumia vifaa hivyo kwa ufasaha.
Baadhi
ya wanachama wa KGPC wakizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo wamesema kuwa
wameupongeza uongozi wa club yao na UTPC kwa kuzingatia na kuona usalama wa
wanachama wao wanapotekeleza majukumu yao ya kikazi katika kipindi hiki cha
mlipuko wa virusi vya corona.
0 Comments