WATU
tisa wamefariki baada ya boti la abiria kuzama katika ziwa
Tanganyika.
Akizungumza
na blog hii kwa njia ya simu Kamanda wa polisi mkoani Kigoma Kamishna Msaidizi Martin
Ottieno amethibitsha kutokea kwa ajali hiyo katika eneo la rasini.
Amesema
kuwa Boti hiyo iitwalo Mv Nzeimana linalofanya safari zake kati ya Kijiji
cha Sibwesa na Ikola limezama likiwa abiria sitini ambapo abiria
hamsini na moja wameokolewa.
“Watu
tisa waliofariki miili yao imeshaopolewa kutoka majini ambapo kati yao wanawake ni saba na
waume wawili, lakini watu 51 wameokolewa wakiwa hai” alisema Kamanda Ottieno
Aidha
Kamanda Ottieno amesema chanzo cha ajali
hiyo ni upepo mkali uliosababisha boti hilo kukosa muelekeo na hatimaye
kupinduka
Baadhi
ya wananchi wa kijiji cha Sibwesa wamesema kuwa kuna baadhi ya miili ya watu
ilisukumwa na upepepo mpaka nchi kavu huku wakisema
“Kulingana
na hali hiyo kwasasa baadhi ya wananchi wa Sibwesa wamekaa vikundi vikundi
kutokana na kupoteza jamaa zao kupoteza uhai”
Nao
baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji akiwemo Josephina Richard na
Samweli Costatine wamesema changamoto za usafiri wa majini zimekuwa nyingi
kutokana na boti kujaza sana abiria sambamba
na mizigo kuwa mingi.
“kwakweli
tunaomba boti za mizigo ziwe za mizigo tu na boti za abiria ziwe za abiria tu
hapo tunaweza kupunguza ajali za majini lakini pia kuwe na vifaa vya kuwasaidia
abiria wakati vyom,bo vinapozama” walisema.
0 Comments