SERIKALI KUJENGA VYUO VYA UFUNDI KATIKA HALMASHAURI NCHINI


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof Joyce Ndalichako akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyamidaho Wilayani Kasulu mkaoni Kigoma kabla ya kuzufungua chuo cha ufundi Stadi VETA kijijini hapo.(Picha na Emmanuel Matinde)


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof Joyce Ndalichako akifungua chuo cha ufundi Stadi VETA katika kijiji cha Nyamidaho Wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof Joyce Ndalichako akikagua chumba kitakachotumika kwa mafunzo ya ushonaji wa nguo.

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof Joyce Ndalichako akikagua chumba cha mafunzo ya komputa, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga.

 Chuo cha ufundi Stadi VETA kilichopo kijiji cha Nyamidaho wilayani Kasulu mkoani Kigoma. 


NA ISACK ARON

WAZIRI wa Elimu Sayansi Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof Joyce Ndalichako ameeleza kuwa serikali imetenga takribani shilingi billion 48 kwaajili ya ujenzi wa vyuo  vya ufundi stadi katika halmshauri ishirini na tisa nchini nzima lengo likiwa ni kuhakikisha kila mkoa unakuwa na vyuo hivyo kufikia mwaka 2025.

 


Waziri Ndalichako alizungumza hayo wakati akizundua chuo cha ufundi stadi VETA katika kijiji cha Nyamidaho wilayani kasulu Mkoani Kigoma kilichogharimu zaidi ya shilingi milioni 400 katika ukarabati wake baada ya kujengwa tangu mwaka 2014 chini ya ufadhili wa shirika la Word Vision.

 

Aidha Waziri Ndalichako ameeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2019/20 tayari vyuo kumi katika halmashauri mbalimbali nchini vimekamilika huku jitihada za kuongeza vyuo vingine zikiendelea kufanywa ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

 

“Tunaendelea na ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika halmashauri 29 nchini ambapo serikali imetenga fedha takribani shilingi milioni 48 kwaajili ya ujenzi huo” alisema Waziri Ndalichako

 

Chuo hicho ambacho kilianza rasmi kuto mafunzo mwezi februari mwaka huu  ikiwemo mafunzo ya umeme,ushonaji na kompyuta kina wanafunzi  62 mpaka sasa lakini inaelezwa kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 600 kwa mafunzo ya muda mfupi na wanafunzi 160 kwa mafunzi ya muda mrefu.

 

Mkuu wa mkoa wa Kigoma  wa Kigoma Brigedia Jenerali Emmanuel Maganga alisema ni jukuma kwa wananchi wa kijiji cha Nyamidaho na mkoa wa Kigoma kwa ujumla kuchangamkia fursa hiyo ili kuweza kujiajiri ajira

 

Chuo cha Ufundi veta katika kijiji cha Nyamidaho wilayani kasulu kinakuwa ni chuo cha pili cha Veta kwa mkoa wa Kigoma na kutoa wigo mpana kwa kusomea mafunzo ya ufundi stadi kwa wakazi wa mkoa huu.

 

 





Post a Comment

0 Comments