WAANDISHI WA HABARI ZA MITANDAONI WATAKIWA KUFUATA MAADILI YA UANDISHI.

Waandishi wa habari za mtandaoni wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kikao cha kutathimini mradi wa utetezi na ushawishi wa haki za binaadam kwa kutumia takwimu(DDA) 

Wakili wa kujitegemea James Marenga akisisitiza jambo kwa waandishi wa  habari za mtandaoni hasa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari kwenye kikao cha tathimini ya mradi wa utetezi na ushawishi wa haki za binaadam kwa kutumia takwimu(DDA)


Mwenyekiti wa Arusha Press Club  Claud Gwandu ambao ndo wasimamizi wakuu wa mradi huo akizungumza wakati wa kikao cha tathimini ya mradi  wa utetezi wa ushawishi wa haki za binaadam kwa kutumia takwimu(DDA). 

Ofisa program wa mradi wa utetezi wa ushawishi wa haki za binaadam kutumia takwimu(DDA)Lina Muro kutoka taasisi za freedom house akichangia mada wakati wa kikao cha tathimini ya mradi wa utetezi wa ushawishi wa haki za binaadam kwa kutumia takwimu

Mratibu wa Arusha press club na ofisa mipango wa mradi Seif Mangwangi akizungumza jambo wakati wa kikao cha tathimini ya mradi.


Na Editha Karlo,Dodoma

WAANDISHI wa habari wa vyombo vya habari mbadala (altenative media) wametakiwa kufuata maadili ya uandishi ikiwemo kuandika habari za ukweli na za uhakika ili kuepuka upotoshaji unaoweza kuleta migogoro.


Wakili wa kujitegemea James Marenga aliyasema hayo jana kwenye ukumbi wa Royal village jijini Dodoma  kwenye kikao cha tathmini ya mradi wa utetezi na ushawishi wa Haki za binaadamu, mradi unaotekelezwa na waandishi wa habari wa vyombo mbadala nchini kutoka mikoa mbalimbali Tanzania bara na visiwani.


Marenga alisema kuwa waandishi wa habari za mtandaoni wanatakiwa kuandika habari kwa usawa na ukweli zaidi kwasababu wamekuwa wakiripoti matukio papo kwa papo ambao hujulikana kama waandishi wa habari za chap chap mtandaoni hivyo wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kusimamia maadili ya uandishi.


Pia aliwataka waandishi wa habari kutokuchanganya uandishi wa habari na siasa, huku akisisitiza kuwa endapo mwandishi wa habari anataka kuwa mwana siasa basi aachane na kazi ya uandishiwa habari.


"Mwandishi wa habari unajihusisha na siasa kupitia labda chama chochote unadhani kupitia uandishi wako unaweza kutendea haki vyama vingine kwenye kazi yako, ukiamua kuwa mwanasiasa kama wewe ni mwandishi wa habari basi huku inabidi utoke, taaluma ya uandishi wa habari ni tofauti na taaluma zingine"alisema

 

Mwenyekiti wa club ya Arusha Press Club Claud Gwandu ambao ndio wasimamizi wakuu wa mradi huo aliwataka wanahabari kufuata sheria zilizopo hata kama hawakubalina na sheria hizo wakati asasi zao zikiendelea kuwasiliana na serikali kuona namna bora ya kurekebisha sheria hizo.


Naye Mwenyekiti wa waandishi wa habari wa vyombo mbadala (Altenartive media) Midraji Ibrahimu aliwasisitiza waandishi wa habari kuzingatia maadili ya uandishi wa habari hususanu katika kipindi hiki tunachoelekea kwenye kampeni na uchaguzi mkuu.


Seif Mangwangi Mratibu wa Arusha Press Club na Afisa mpango wa mradi huo alisema kuwa miongoni mwa malengo ya kikao hicho ni kupitia mafanikio,changamoto pamoja na matarajio ya baadae ya mradi toka ulipoanza Machi 2019.


Alisema pia wanakikundi wanatakiwa kutunga kanuni zao ambazo zitakuwa kama mwongozo zitakazosimamia kundi hilo la waandishi wa habari za mtandaoni.


Seif alisema kikao hicho ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa utetezi na ushawishi wa haki za binaadam kwa kutumia takwimu(DDA)kupitia vyombo vya habari mubadala(Altenartive media) unaofadhiliwa na mfuko wa maendeleo wa watu wa marekani kupitia taasisi za freedom house pamoja na PACT na una simamiwa na club ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Arusha.

Post a Comment

0 Comments