WATU SABA WASHIKIRIWA NA POLISI KWA KOSA LA KUFANYA VURUGU KIGOMA




Nyumba ya Mwandishi wa habari wa kujitegemea Joctan Maganga baada ya kuharibiwa na wananchi.

JESHI la polisi mkoani Kigoma linawashikilia watu saba ambao ni wakazi wa kata ya Mwanga Kusini ndani ya  Manispaa ya Kigoma ujiji mkoani Kigoma kwa tuhuma za kufanya fujo na uhalibifu wa nyumba pamoja na  uporaji wa vitu mbalimbali vyenye thamani .

Kamanda wa polisi mkoani hapa ACP James Manyama alieleza tukio hilo lilitokea hivi karibuni kuwa chanzo chake ni wananchi kumtuhumu Joctan Maganga ambaye ni mwandishi wa habari wa  kujitegemea kuhusika katika upoteaji  wa jirani yake Philipo Hussein mwenye umri wa miaka 21.

Ndugu wa kijana huyo ambaye anaelezwa kupotea  kwa takribanii siku saba wanaeleza kuwa kulikuwa na mahusiano ambayosi mazuri kati ya kijana huyo pamja na Jocta Maganga amabye anatuhumiwa kumteka ambapo inasemkana walikuwa wakigombania mpaka wa ardhi kwa zaidi ya mwaka sasa hapo awali.

Aidha katika tukio hilo askari wawili wa jeshi la polisi mkoani hapa walijeruhiwa wakati wakijaribu kuzuia  vurugu na uharabifu wa nyumba ambayo vitu mbalimbali viliibiwa na wanannchi  wenye asira kali.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani hapa lilimkamata mtuhumiwa mmoja mwanaume ambaye jina lake  limehifadhiwa akiwa na silaha moja ain ya AK-47 ikiwa na magazine moja yenye risasi 30 katika kata ya kalinzi  wilaya ya kigoma vijijini.

 



Post a Comment

0 Comments