WAZEE KIBONDO WAPEWA VIFAA VYA KUOSHEA MAGARI ILI WAJIKWAMUE KIUCHUMI

Baadhi ya wazee wilayani Kibondo wakiwa na vifaa vya kuoshea magari walivyokabidhiwa na shirika la Help Age International. (Picha Na James Jovin)

Vifaa vya kuoshea magari vilivyotolewa kwa wazee wilayani Kibondo kwa lengo la kujikwamua kiouchumi. ( Picha Na James Jovin)

SHIRIKA la Help age International wilayani Kibondo mkoani Kigoma limetoa vifaa mbali mbali vilivyogharimu zaidi ya shilingi milioni tano  vitakavyowasaidia wazee kuanzisha mradi wa kuosha magari na hivyo kujipatia kipato kitakachowasaidia kujikimu katika maisha


Akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa hivyo Afisa Ujasiliamali wa Shirika la Help age wilayani Kibondo bw. Elisante Kiraha alisema kuwa vifaa hivyo vimetolewa kufuatia maombi ya Kikundi cha Uchumi cha Wazee Kibondo walioomba kuanzisha mradi wa kuosha magari ili kujikimu kimaisha


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Wilaya ya Kibondo bw. Fransis Mkosamali na Katibu wa baraza hilo Bw. Gidion Menyo wameshukuru kwa msaada huo na kwamba watahakikisha mradi huo unakuwa mkubwa na kusaidia wazee wote hasa wale wenye mahitaji maalumu na wasio jiweza.

 

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya ya Kibondo Bw. Jamhuri Kidumu pamoja na Afisa Usatawi wa Jamii Bi Sophia Gwamagobe wamewapongeza wazee hao kwa kuanzisha mradi ambao utawasaidia katika maisha lakini pia shirika la Help Age kwa kuwa karibu na wazee siku zote.

 


Post a Comment

0 Comments