WAZIRI MKUU APOKEA SALAMU ZA POLE KUTOKA BURUNDI

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja  na Waziri Mkuu  wa Burundi Jenerali Alain Guillaume , Leo Julai 27, 2020, Jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Waziri. Mkuu)



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri Mkuu wa Burundi Jenerali Alain Guillaume (Kushoto). Waziri Mkuu wa Burundi alifika leo Julai 27, 2020  Ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais na Wananchi wa Jamhuri ya Burundi  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na watanzania kufuatia kifo cha Rais wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa, Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifanya mazungumzo na Waziri Mkuu  wa Burundi Jenerali Alain Guillaume, Leo Julai 27, 2020, Jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Waziri. Mkuu)



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hii leo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Burundi Jenerali Alain Guillaume, Ofisi ndogo za Waziri Mkuu, Magogoni Jijini Dar es Salaam

 

Katika mazungumzo hayo Jenerali Alain aliwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais na wananchi wa Jamhuri ya Burundi  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na watanzania kufuatia kifo cha Rais wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa.

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa hatua hiyo inathibitisha udugu uliopo kati ya Tanzania na Burundi katika vipindi vyote vya majonzi na furaha

 


Post a Comment

0 Comments