Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Burundi Jenerali Alain Guillaume , Leo Julai 27, 2020, Jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Waziri. Mkuu) |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Burundi Jenerali Alain Guillaume, Leo Julai 27, 2020, Jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Waziri. Mkuu) |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hii leo amekutana na kufanya
mazungumzo na Waziri Mkuu wa Burundi Jenerali Alain Guillaume, Ofisi ndogo za
Waziri Mkuu, Magogoni Jijini Dar es Salaam
Katika
mazungumzo hayo Jenerali Alain aliwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais na wananchi
wa Jamhuri ya Burundi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli na watanzania kufuatia kifo cha Rais wa Awamu ya Tatu
Benjamin William Mkapa.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa hatua hiyo inathibitisha udugu uliopo kati ya
Tanzania na Burundi katika vipindi vyote vya majonzi na furaha
0 Comments