Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akisisitiza
jambo wakati akizungumza kwenye maonesho ya kilimo yaliyoandaliwa na Taasisi ya
Utafiti wa Kilimo-TARI SERIAN Jijini Arusha
Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akikagua shamba la maharage wakati alipotembelea Jijini Arusha kufungua maonesho ya kilimo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo-TARI SERIAN Jijini Arusha |
RAIS wa awamu ya tatu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Benjamini Mkapa wakati wa utawala wake aliainisha kuwa nia na
lengo kuu la sekta ya kilimo ni
pamoja na kuhakikisha wakulima wa Tanzania
wanapata elimu na ujuzi wa kutosha wa vitendo, hivyo Wizara ya Kilimo inatakiwa
kujizatiti kikamilifu kuwasaidia wakulima kuishi katika uchumi wa viwanda.
Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga alibainisha hayo hivi karibuni
wakati akizungumza kwenye maonesho ya kilimo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti
wa Kilimo-TARI SERIAN Jijini Arusha na kuongeza kuwa Mkapa alieleza dhamira ya
serikali kuhakikisha kuwa inafikia uchumi wa kati na wa viwanda kwa
kuwa na uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo.
“Hayati Rais Mkapa wakati wa utawala wake alilisisitiza kuwa
nchi yoyote ili iwe na Usalama na Amani ni lazima wananchi wawe wamejitosheleza
kwa chakula endapo kutakuwa na upungufu wa chakula ni dhahiri kuwa nchi haiwezi
kuwa na utulivu wa kisiasa na kimaendeleo’’ Alisema
Pia Hayati Mkapa alipiga vita kwa nguvu kubwa umasikini ambapo
alianzisha kauli mbiu ya MTAJI WA MASIKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE ikilenga
kuhamasisha wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kuchagiza shughuli za
maendeleo.
Kadhalika Hayati Benjamin Mkapa alisisitiza ulazima wa maafisa
Ugani kufanya kazi mashambani kwa wakulima badala ya kuishi mjini pekee kwani
kwa kufanya hivyo watawasaidia wananchi kunufaika na kilimo kwa kuwa na tija
kubwa katika uzalishaji hivyo kuwa na kilimo cha kibiashara.
Waziri Hasunga alisema kuwa Hayati Rais Mkapa alikuwa muumini wa
teknolojia bora za kilimo hivyo aliitaka Wizara ya Kilimo kuhakikisha kuwa
inatumia teknolojia na zana bora za kilimo ili kuhakikisha kuwa malighafi
zinazotokana na mazao ya kilimo zinaendelea kuzalishwa kwa wingi.
Kadhalika, Hayati Mkapa alisema kuwa kilimo bila utaalamu
hakiwezi kumkomboa mkulima hivyo aliagiza Taasisi za utafiti wa Kilimo na vyuo
vya mafunzo ya ufundi kuhakikisha kuwa vinaendeleza juhudi za kuimarisha elimu
kwa wananchi na wakulima ili kuwa na taifa bora lenye wakulima wazuri.
0 Comments