WIZARA YA AFYA YAZINDUA KAMPENI YA JAMII KUPAMBANA NA CORONA

Magari maalum yaliyoandaliwa kwaajili ya kampeni ya kuhamasisha jamii kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa wa Corona. (Picha Na Isaac Aron Isaac)


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt Simon Chacha akikabidhi vipeperushi kwa baada ya wananchi watakaoshiriki kwenye kampeni hizo. (Picha Na Isaac Aron Isaac)


WIZARA ya afya kupitia kitengo cha elimu ya afya kwa umma imezindua rasmi kampeni ya kuhamasisha jamii  kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa wa Corona kwa mikoa 14 nchi nzima kwa kufuata taratibu zote zilizowekwa na wataalamu wa afya na serikali.

Kampeni hiyo inaelezwa kufika katika maeneo yote ya mikoa hiyo kwa siku 30 kwa kila mkoa ambapo licha ya ugonjwa huo kuelezwa kupungua kwa kiasi kikubwa bado nchi jirani zinakabiliwa na ugonjwa huo hivyo kuendelea kuhamasisha jamii kuchukua tahadhari.

Dkt Hamesha Chinyuri kutoka idara ya kinga kitengo cha elimu ya afya kwa umma anasema kwamba kampeni hiyo itaendeshwa kiupitia magari maalum ambayo yatakuwa yanapita katika mitaa mbalimbali kuendelea kutoa elimu.

Akizundua kampeni hiyo kwa Mkoa wa Kigoma Mganga mkuu mkoani hapa ameeleza kuwa kampeni hiyo itakuwa chachu ya kusaidia wananchi kuendelea kujikinga na magonjwa mengine ikiwemo ugonjwa wa malaria ambao umekuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi mkoani Kigoma.

Katika kampeni hiyo wizara ya afya kupitia kitengo cha elimu kwa umma inashirikilia na shirika la msalaba mwekundu katika kutoa elimu ya uhamasishaji kwa wananchi kuendelea kujikinga na ugonjwa wa corona.

 



Post a Comment

0 Comments