Naibu waziri wa Ujenzi Mhandisi Elias Kwandikwa akikagua ujenzi wa barabara ya Simba Kalya mara baada ya kutembelea vijiji hivyo. (Picha NA Isaac Aron Isaac) |
Baadhi ya wananchi wa Vijiji vya Simbo Kalya wakiendelea na shughuri zao kwa kutumia barabara ambayo inaendelea kujengwa. (Picha Na Isaac Aron Isaac) |
Barabara ya Simbo Kalya inayojengwa kwaajili ya kuondoa adha ya usafiri kwa wakazi wa vijiji hivyo. (Picha Na Isaac Aron Isaac) |
Na Isaac Aron Isaac,
Kigoma
Wakazi wa vijiji
vya kusuni mwa ziwa Tanganyika Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma wameiomba serikali
kufanya marekibisho ya miundombinu ya usafiri kuelekea katika vijiji hivyo ili
kuepuka adha pamoja na vifo vitokanavyo na changamoto ya usafiri.
Wameeleza hayo katika ziara
ya Naibu waziri wa Ujenzi Mhandisi Elias Kwandikwa alipotembela barabara ya
Simbo Kalya yenye urefu wa kilometa takrabini 230 ambayo licha ya
kujengwa kwa kiwango cha vumbi bado imekuwa na tatizo kwa wananchi wa meneo
hayo.
Kwa mujibu wa wananchi
hao kuanza Mwezi Januari mwaka huu vifo kadhaa vimeripotiwa mpaka
sasa katika ziwa Tangayika kwa upande wa kusini ambapo
wakazi wake wanaeleza kuwa ni kutoka na changamoto ya usafiri ambayo
imekuwa ikiwalazimu kupanda maboti ambayo si salama kwa uhai wao.
Aidha Meneja wa Tanroad
mkoani Kigoma Mhandisi Narsisi Choma ameeleza kuwa kwasasa ukarabati unaendelea
katika maeneo ambayo yaliingiliwa na maji kutoka ziwani ambapo tayari serikali
imetoa fedha kwaajili ya ujenzi barabara katika kijiji cha Sibwesa
ambapo kuna changamoto kubwa zaidi.
Kwa upande wake Naibu
Waziri Mhandisi Elias Kwandikwa aliwatoa hofu wakazi wa maeneo hayo na
kusisitiza kuwa maboresho hayo ya yatahusisha ujenzi kwa kiwango cha Rami ili
kusaidia pia katika shughuli za kiuchumi na kibiashara katika maeneo hayo ambayo
shughuri za kimaendeleo zinakwama kutokaa na ubovu wa barabara.
Hata hivyo Barabara ya
Simbo Kalya ilianza kujengwa mwaka 2012 chini ya Tanroad baada ya kutokuwepo
hapo awali lakini bado wananchi wa maeneo hayo wanaeleza
kuwa wao hujisikia amani zaidi wakipanda usafiri wa majini zaidi ya barabara.
0 Comments