bi. Evodia Pius mhanga wa wizi huo (picha na James Jovin )
KAKONKO
Taasisi ya
kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU wilayani Kakonko mkoani Kigoma
imefanikiwa kurudisha fedha kiasi cha shilingi milioni 54 za mwalimu mstaafu alizokuwa amedhulumiwa na
mkopesha liba miaka sita iliyopita
Kamanda wa
taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa wilayani kakonko bw. Ladislaus Ibrahimu
akizungumza na KGPC Blog amesema kuwa aliyekuwa
ameibiwa ni bi. Evodia Pius aliyekuwa akifundisha shule ya msingi Kasanda baada
ya kukabidhi kadi ya benk kwa mkopesha liba aliyeamua kuhamisha fedha hizo
kiasi cha shilling milioni 54
Amesema kuwa
bi. Evodia alistaafu kazi mwaka 2014 na kupewa pensheni ya milioni 70 lakini
baada ya kustaafu alidanganywa na mkopesha liba ambaye hakutajwa jina lake
ambaye alimkopesha kiasi cha shilingi milioni saba ili aweze kujenga nyumba
kisha akamuibia mama huyo kiasi cha shilingi milioni 54 katika akaunti yake ya
benki na kuzihamishia katika akaunti yake binafsi
Aidha bi.
Evodia ambae alikuwa mwalimu wa shule ya msingi Kasanda amesema kuwa
aliyesaidia kupatikana kwa fedha hizo ni mwanae wa kike ambaye wakati zinaibiwa
alikuwa bado mdogo na ndipo baada ya miaka sita kupita alipata ufahamu na aliamua kuomba msaada kwa mkuu wa wilaya ya
Kakonko kanali Hosea Ndagara ambaye baadae aliagiza taasisi ya kupambana na
rushwa TAKUKURU kufuatilia sakata hilo na waliweza kufuatilia kwa kina na
kugundua kuwa fedha hizo ziliibiwa na mtu aliyekuwa amemkopesha mama yake kwa
liba miaka sita iliyopita.
Mkopeshaji liba
huyo ambaye hakutajwa jina lake kwa sababu za kiusalama alikili kufanya hivyo
na ndipo ameweza kutoa shilingi milioni kumi za awali na fedha zote zilizobaki
atazilipa kila mwezi na kufikia mwisho wa mwaka huu wa 2020 ameahidi atakuwa
amemaliza kurudisha fedha zote mali ya bi. Evodia
Kwa upande
wake mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama na mkuu wa wilaya ya Kakonko
Kanali Hosea Ndagara amemtaka mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya
Kakonko kuendesha semina kwa wafanyakazi wote juu ya tatizo hili la mikopo ya
liba linaloendelea kushamili kila siku huku watumishi walio wengi hasa wastaafu
wakiibiwa fedha zao kila kukicha. ENDS
1 Comments
Wamefanya jambo la kheri Mungu amsaidie sana bi evodia na wafanyakazi wengine yujifunze mikopo.hiyo isio salama
ReplyDelete