Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene akizungumza na wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene akicheza ngoma ya Kirundi sambamba na wacheza ngoma hiyo ambao pia ni wakimbizi. |
Na Mwandishi Wetu, Kasulu Kigoma
SERIKALI imesema itatumia nguvu kubwa katika kudhibiti raia wa Burundi wanaoingia nchini na baadaye kuingia katika maeneo ya msitu wa hifadhi wa Makere Kusini na Kaskazini uliopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma na kufanya uharibifu mkubwa na kufanya kilimo cha bangi.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene, alisema hayo wakati wa ziara yake mkoani Kigoma wakati
akizungumza na wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu, ambapo pia
alieleza hatua mpya zitakazoanza kuchukuliwa kwa wakimbizi wasiokuwa na vibali
vya kuwa nchini.
“Kuanzia
sasa utaratibu uliokuwa unatumika wa kuwarejesha wale waliokuwa wanakamatwa
bila vibali wakiwa wametoroka kwenye makambi hautafanyika tena ila tutafanya
mchakato wa kisheria wa kuwa tunawapeleka gerezani, utaratibu wa kutopelekwa
magerezani nimeufuta kuanzia sasa tutawapeleka huko, hatuwezi kuvumilia hali hiyo”
alisisitiza Waziri Simbachawene.
Wakati
huo huo Waziri Simbachawene alisisitiza kuwa Tanzania haitatoa tena uraia kwa
wakimbizi kutoka Burundi na kuwataka warejee nchini kwao huku Balozi mdogo wa
ubalozi wa Burundi mkoani Kigoma Kabura Cyriaque, akiwataka warundi warudi
nyumbani na kwamba serikali yao ni serikali mzazi wa kila raia wa Burundi.
“Kile
kilichotokea cha kutoa uraia wa jumla kwa idadi kubwa hakitatokea tena kwasababu hata wale ambao
walipewa uraia wamebakia makambini hawajaenda kuchanganyikana huko kwenye
jamii, kila mtu akitoka hapa wazo lake liwe ni kurudi nyumbani” alisema Waziri
Simbachawene.
“Kama
tulivyowaambia serikali iliyoko madarakani kwasasa ni serikali mzani nan i serikali
inayofanya kazi” alisema Barozi Mdogo wa Burundi.
Awali
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Simon Anange, alimueleza Waziri Simbachawene
kuwa maeneo mengi ya Wilaya ya Kasulu, yamejaa wahamiaji haramu ambao baadhi
yao huingia katika msitu wa hifadhi ya Makere wakijifanya wanalima kumbe
huficha silaha ambazo huzitumia kufanya uhalifu.
“Kwa
uchunguzi wetu katika kijiji cha Kitanga ambapo ndio tunapakana na Burundi ndio
sehemu ambayo siraha nyingi zinaingia kutoka Burundi, yani watu wanaotoka
Burundi wakiingia Tanzania wanabadirishana Sub machine gun na gunia moja la
mahindi au la maharage” alisema Kanal Anange
0 Comments