TRA KIGOMA YAJA NA KAMPENI YA MLANGO KWA MLANGO

 

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Kampeni ya Utoaji Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakati walipomtembelea ofisini kwake ajili ya utambulisho kabla ya kuanza Kampeni ya kutoa elimu kwa Mlipakodi (mlango kwa mlango) mkoani hapo.


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye akiongea na kutoa baraka zake kwa timu ya Maafisa wa Kampeni ya Utoaji Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kabla ya kuanza kwa kampeni ya Elimu kwa Mlipakodi (Mlango kwa Mlango) inayoanza leo 17 hadi 30 Agosti, 2020 mkoani Kigoma.


Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kigoma, Bw. Jackob Mtemangombe akitoa utambulisho mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye kuhusu ugeni wa timu ya Maafisa wa Kampeni ya Utoaji Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA ambao wapo kwa ajili ya Kampeni ya kutoa elimu kwa Mlipakodi (mlango kwa mlango) mkoani hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye akiongea na kutoa baraka zake kwa timu ya Maafisa wa Kampeni ya Utoaji Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kabla ya kuanza kwa kampeni ya Elimu kwa Mlipakodi (Mlango kwa Mlango) inayoanza leo 17 hadi 30 Agosti, 2020 mkoani Kigoma
Maafisa wa Kampeni ya Utoaji Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiwa ndani ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma wakati walipomtembelea kwa ajili ya kujitambulisha kabla ya kuanza kwa zoezi la utoaji elimu kwa Mlipakodi (mlango kwa mlango) mkoani hapo.


Na Magreth Magosso,Kigoma

 

MAMLAKA ya Mapato (TRA)  imetambulisha Kampeni ya utoaji Elimu kwa Mlipa kodi  ya Mlango kwa Mlango kwa Mkuu wa Mkoa Thobiasi Andengenye ikiwa ni kampeni itakayo dumu kwa  wiki mbili katika halmashauri za mkoa huoa.

 

Akitambulisha Kampeni hiyo  leo katika ofisi ya Mkuu  huyo wa Mkoa, Meneja wa TRA Kigoma  Jacob Mtuman'gombe alisema lengo ni kuwafikia wafanyabiashara kwa urahisi kuliko semina zilizozoeleka ambapo wengi hawafiki kupata elimu sahihi ya ulipaji kodi.

 

"Vigumu walipa kodi kufunga maduka na kuja kwenye semina, zoezi la mlango  kwa mlango ni fursa ya kupanua uelewa kwao na wao kutupa changamoto zao na kutathimini ufanyaji kazi wao hivyo nawasihi wasikimbie wahusika wapo kwa ajili ya kuwaelimisha na si vingine" alisisitiza Mtuman'gombe.

 

Alisema timu ya maofisa elimu ya mlipaji kodi kutoka makao makuu watashirikiana na maofisa wa mkoani humo ikiwa ni moja ya mkakati wa mamlaka katika kurahisisha zoezi la utoaji wa elimu kwa wadau wao ndio sababu ya kuomba ridhaa kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma ili abariki zoezi hilo litakalo dumu kwa wiki mbili katika wilaya mtambukwa kwa maslai mapana ya jamii na Taifa  kiujumla.

 

Aidha amekiri zoezi hilo kuwa chachu kwa wakwepa kodi kutambua wajibu wao na mamlaka kubaini kero zao kwa  kutathimini biashara zao kwa malipo  stahiki ya kodi.

 

Akipokea  ombi hilo Mkuu wa mkoa huo Tbobias Andengenye alisema atahakikisha taasisi zote zinawapa ushirikiano kwa lengo la kuboresha ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla .

.

"Siku zote ukitumia nguvu kudai haki haisaidii zaidi ya migogoro lakini kitendo cha kumpa elimu sahihi Mwananchi ni chachu ya mabadiliko tarajiwa hivyo tumieni elimu hiyo kwa matokeo chanya"alisema.

 

Aidha Andengenye amewakumbusha maofisa wa TRA kutumia vyema sheria ya kodi kwa hekima na busara ili kuondoa mikwaruzano baina  ya wafanyabiashara na serikali huku akitolea mfano wa baadhi ya wafanyabiashara kuacha kuratibu bidhaa zao hapa mkoani na  kwenda mikoa jirani kuratibu bidhaa hizo jambo ambalo ni dalili ya shida ya tafsiri ya sheria ya ulipaji kodi.

 

Alishauri kutoza kodi kwa weledi ili kuwapa fursa wafanyabiashara wadogo wakati na wakubwa kulipa kodi kwa hiari kwa maendeleo ya nchi ambayo inategemea fedha za ndani kukamilisha miradi husika.

 

Akizungumza na Kgpc blog mfanyabiashara wa  Soko  la kigoma mjini Prisca David alikiri TRA haina shida na mtu endapo utakuwa na leseni ya biashara,  Mashine ya kieletroniki ambayo inatoa risiti kulingana na mauzo na kushauri wanaotumia njia za panya waache.

 

Naye Deudatius Vuma mfanyabiashara soko la kigoma mjini alisema kitendo cha TRA kuwafuata wadau wao ni la kupongezwa na si la kubezwa huku akiongeza kuwa nchi inaenda kwa kasi katika kuboresha huduma za jamii katika miradi ya Umma hivyo wafanyabiashara wawe wakweli katika biashara zao.

Post a Comment

0 Comments