vifo vya akina mama na watoto vyapatiwa mwarobaini , Nyaruyoba

 



Na James Jovin

KIBONDO

Halimashauri ya wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma iko katika hatua za mwisho za umaliziaji wa kituo cha afya katika kata ya Nyaruyoba kituo ambacho kitaghalimu  zaidi ya milioni mia tatu mpaka kukamilika kwake ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuboresha huduma za afya

 

Hayo yamebainishwa na Dr. Laurian  Kanaganwa wakati akimwakilisha mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya Kibondo katika ukaguzi wa shughuli hiyo na kwamba ujenzi umefikia asilimia tisini mpaka sasa

 

Aidha amesema kuwa kukamilika kwa kituo hicho cha afya kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza vifo vya akina mama na watoto vilivyokuwa vikitokea kutokana na ukosefu wa huduma za afya na kutembea umbali mrefu katika kutafuta matibabu

Katika hatua nyingine Dr. Kanaganwa amesema kuwa mradi huo wa kituo cha afya unatekelezwa kwa kutumia force account na unatarajiwa kumalizika ndani ya miezi mitano, mpaka sasa mradi huo umeghalimu fedha za kitanzania million 239.7 ambapo salio ni shilingi milioni 60.2 wakati ujenzi umefikia asilimia 90

 

Nao baadhi ya wananchi wa kata ya Nyaruyoba wameipongeza serikali kwa hatua hiyo na kwamba walikuwa wakilazimika kutembea umbali mrefu kutafuta huduma katika kituo cha afya Kifura au hospitali ya kibondo hivyo kukamilika kwa kituo hicho ni hatua kubwa ya maendeleo katika kata yao. ENDS

Post a Comment

0 Comments