Bi.Mwanayasha Hamis akiwa amebeba wanae mapacha wakifurahia zawadi ya godoro na kitanda walichokabidhiwa na waumini wa Kanisa la African Inland Mkoa wa Kigoma.kama sehemu ya huduma ya idara ya huduma ya mama na mtoto kwa kanisa hilo. (Picha na Magreth Magosso Kigoma) |
Na
Magreth Magosso, Kigoma
WAUMINI
wa Kanisa la African Inland (AICT) Mkoa wa Kigoma wamefanikiwa kuwapa na kuwaongezea
faraja watoto 15 waishio katika mazingira magumu baada ya kuwakabidhi vitanda
na magodoro.
Zawadi
hizo zimekabidhiwa jana baada ya ibada ya kubariki watoto katika kanisa hilo
ukiwa ni mpango wa kutimiza ndoto za watoto waishio katika mazingira
magumu na kuwezeshwa usingizi mororo kupitia kitanda na godoro zuri kwa usalama
wa afya zao.
Akifafanua
hilo Mratibu wa Kituo cha huduma ya mama na mtoto AICT Kigoma Robart Chamungu
alisema kituo kina watoto 247 lakini magodoro 15 na vitanda 15 ni kwa ajili ya
watoto wenye uhitaji wa vifaa hivyo.
"Tunalea
watoto wenye mazingira magumu kwa lengo la kupunguza changamoto zinazowakabili
katika familia wanazoishi na kati ya watoto 247, watoto 15 tu watanufaika
na msaada huu huku wengine wakinufaika na vyakula vya msingi ambapo kila mwisho
wa mwezi wanapewa mahitaji yao ya msingi."alisema Mratibu wa kituo
hicho.
Alieleza
kuwa kupitia mpango wa mwaka wa fedha wa 2020/21 kwa mashirikiano na
washirika wenza Asasi ya Compassion yenye makao yake mkoani Arusha wataendelea
kupunguza changamoto za watoto waliosajiliwa katika kituo hicho kulingana na
bajeti yao.
Alisema
huduma zingine wanazotoa kwa watoto wa kituo hicho ni pamoja na elimu ya
roho na elimu ya dunia sanjari na matibabu ikiwa ni mkakati wa kuwafariji
watoto wenye mazingira magumu.
Akikabidhi
vifaa hivyo Askofu Silasi Kezakubi wa Dayosisi ya Tabora aliwasihi waumini wa
madhehebu hayo wamtumikie mungu kwa ajili ya kanisa na watu wenye uhitaji.
"Nipo
katika ziara ya mkoa wa Kigoma na kesho Katavi lengo kuzungumza na
wakristo, kuokoka ni kujitoa kwa kutoa zawadi kwa wengine. Hakuna mtu asiyeweza
kusaidia mwingine, wanaotoa wengi ni watu wenye maisha ya kawaida” alisema
Aidha
ameikumbusha jamii isimamie misingi ya malezi ya watoto wote bila kubagua, kitendo
cha kumnyoshea kidole mtoto wa mwenzako kwa tabia mbovu sio suluhisho badala
yake umkanye kwa kumuelimisha athari ya vitendo viovu kwake na jamii kwa
ujumla.
Hata
hivyo KGPC Blog imezungumza na Mwanayasha Hamisi ni miongoni mwa wanufaika
15 wa zawadi hizo, alisema hana cha kuwalipa zaidi ya kuwakabidhi mikononi mwa
Mungu wazidi kubarikiwa na kazi za mikono yao.
Naye
Rebeka Mihuri ni mmoja wa wanufaika wa huduma ya Mama na Mtoto alikuwa na haya “nasaidiwa
na Kanisa la African Inland Mkoa wa Kigoma kwa malazi, chakula, elimu, matibabu
ya afya hatimaye leo napewa godoro kwa kuwa kitanda tulikuwa nacho nyumbani,
nawashukuru”.
Mwisho.
0 Comments