Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa akionyesha fomu ya kugombea ubunge katika jimbo la Ruangwa mkoani Lindi. |
Na Mwandishi Wetu, Lindi
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Leo Agosti 21, 2020 amechukua fomu ya kugombea
ubunge katika jimbo la Ruangwa Katika mkoa wa Lindi kupitia Chama cha Mapinduzi
(CCM).
Waziri Mkuu amekabidhiwa
foam hiyo katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa Wilaya hiyo ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ruangwa
Bw. Frank Chonya.
Baadaya tukio hilo Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa alishiriki sala ya Ijumaa na waumini wa Dini ya Kiislam
katika msikiti wa Nnur uliopo wilayani Ruangwa.
0 Comments