MKUU WA MKOA KIGOMA AAGIZA KUREKEBISHWA KWA UJEZI WA SHULE

 

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishina wa Polisi Thobias Andengenye

Na Isaac Aron Isaac, Kigoma

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina wa polisi (CP) Thobias Andengenye ameeleza kutoridhishwa na ujenzi wa shule ya msingi ya mfano ya Bwega inayojengwa wilayani Buhigwe mkoani kigoma kwa gharama ya shilingi million 700.

Awali ujenzi wa shule hiyo ulipigiwa kelele na waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako alipotembelea mradi huo mwezi October mwaka jana kwa kushindwa kufuata taratibu za ujenzi ambapo pia aliagiza kurekebishwa kwa ramani lakini hadi sasa suala hilo halijafanyiwa kazi.

Mradi huo unahusisha ujenzi wa vyumba 17 vya madarasa ambapo  kwa sasa ujenzi wake unaendelea licha ya kupigiwa kelele na viongozi kadhaa kwa kushindwa kuendana na hali halisi ya ujenzi wa majengo ya shule za serikali.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma CP Thobias Andengenye naye akasisitiza ramani ya ujenzi wa vyumba vya ofisi ya waalimu na jengo la jiko kuerekebishwa kabla ya wanafunzi kuanza kupata huduma katika  shule hiyo.

“Ofisi ya walimu inatakiwa kuangalia madarasa ili wanafunzi kuwa na nidhamu muda wote wakijua waalimu wanawatazama, huwezi kujenga ofisi ya Mkuu wa Shule ambayo imeyapa mgogo madarasa” alisema Mkuu wa Mkoa Andengenye

Post a Comment

0 Comments