WANUFAIKA WA TASAF WASIFU MPANGO HUO



Na Emmanuel Matinde, Kigoma

Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini, TASAF, kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, wamesifu mpango huo ulivyosaidia kuwatoa katika hali ya umasikini uliokithiri na kuweza kuboresha hali yao ya maisha.

Lonka Musa Lonka na Anezia Benedicto wakazi wa Kijiji cha Mkongoro katika halmashauri ya wilaya ya Kigoma, ni baadhi ya walengwa walionufaika na mpango wa TASAF, na walieleza kuwa awali walikuwa na maisha magumu ila baada ya kupokea pesa walianza kujenga na sasa wanaishi kwenye nyumba nzuri.

“Wakati wa mvua tulikuwa tunapata shida sana kutokana na nyumba kuvuja, lakini kwasasa tunaishi kwenye nyumba nzuri na watoto wanaeda shule bila kuwa na madeni ya ada, tunaishukuru sana TASAF kwa kutubadirilishia maisha” walisema

Abihudi Abeli ni Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Mkongoro, wao wamezungumzia mabadiliko aliyoyashuhudia kwa walengwa wa TASAF kijijini hapo, huku Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Angela Petro akieleza kuwa elimu iliyotolewa kwa walengwa kabla kupokea ruzuku ya TASAF, imesaidia fedha kutumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Awali watu walikuwa nakosa hata mlo mmoja kwa siku lakini baada ya TASAF watu wanakula kuanzia milo miwili hadi mitatu inategemeeana na jinsi mtu alivyojipanga kupitia ile pesa aliyoipata kupitia mfuko wa TASAF” alisema.

Kijiji cha Mkongoro kina watu zaidi ya elfu kumi na tatu, ambapo mpaka sasa wanufaika wa mpango wa TASAF ni 205.


 


Post a Comment

0 Comments