WAFANYABIASHARA KIGOMA WATAKIWA KURASMISHA BIASHARA

Na Tryphone Odas, Kigoma

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Kamishna wa Jeshi la Polisi,  Thobias Andengenye amewataka wafanyabiashara wa Mkoa huu kurasimisha biashara zao kwa wakala wa usajili wa  Biashara na Leseni (BRELA) ili kila mfanyabiashara aweze kufanya biashara bila kusumbuliwa na kudhibiti biashara ambazo sio rasmi.

Amesema hayo wakati akifungua mafunzo kwa Maafisa Biashara  wa Mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi yaliandaliwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Brela yakilenga kuwajengea uwezo wa namna ya kusajili biashara za wafanyabiashara  kwa njia ya mtandao.

“Watu wamekuwa na hofu ya kuanzisha biashara kutokana na mambo mengi wanayotakiwa kuyafanya hivyo serikali kwa kuliona hilo na kupitia BRELA imeamua kurahisisha jambo hili ili kumfanya mtu mwenye nia ya kufanya biashara aweze kufanya biashara” alisema Kamishina Andengenye.

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Kamishna wa Jeshi la Polisi,  Thobias Andengenye. (Picha na Tryphone Odace) 

Afisa Rasilimali watu kutoka Wakala wa Usajili Biashra na Leseni Bw. Migisha Kahangwa alisema mfumo huo utasaidia wafanyabishara kuondokana na usumbufu wa kutumia gharama kubwa kwenda kutafuta hudama za usajili.

“Lengo ni kulasimisha biashara na kuwawezesha wananchi kupunguza gharama na kuweza kuwa rasmi katika kuendesha biashara zao” aliongeza Bw. Kahangwa.

Kwa upande wake Afisa Biashara wa Mkoa wa Kigoma, Deogratias Sangu, alisema mfumo huo utasaidia wafanyabiashara wengi kujisajili kwani kuondoa wimbi la wafanyabiashara ambao sio rasmi kutokana na mkoa huu kupakana na  Nchi nyingine.

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Kamishna wa Jeshi la Polisi,  Thobias Andengenye akiwa  katika picha ya pamoja na maofisa biashara na Tehama kutoka mkoani Tabora, baada ya ufunguzi wa mafunzo ya mtandao ya urasmishaji biashara. (Picha na Magreth Magoso)

Baadhi  ya maafisa biashara akiwemo Bi. Imelda Ukololo na Godfrey Selestine walisema kwa kipindi cha nyuma hawakuwa na uwezo wa kusajili viwanda kwa mfumo wa kawaida na hivyo mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha na kutoa leseni zinazopatikana kwa njia ya mtandao kwa urahisi.

 


Post a Comment

0 Comments