WAKAZI KAKONKO KUNUFAIKA NA MRADI WA HOSPITALI MPYA YA WILAYA

 

Hospitali ya wilaya ya Kokonko inayojengwa katika kijiji cha Itumbiko.

Mkuu wa Wilaya ya  Kakonko Kanal Hosea Ndagala akizungumzia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko.( Picha Na Mwajabu Hoza)

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma Stephano Mag'hanila.

Na Mwajabu Hoza , Kakonko - Kigoma 

WAKAZI zaidi la laki mbili wa wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma wanatarajia kunufaika na ujenzi wa mradi wa Hospitali ya wilaya mradi ambao utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 1.5.

Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya hiyo Kanal Hosea Ndagala amesema Ujenzi huo unatekelezwa katika Kijiji cha Itumbiko ndani ya wilaya ya Kakonko ambapo  hadi sasa umefikia katika hatua nzuri za ujenzi wake.


Aidha hadi sasa  majengo yanayoendelea na ujenzi ni  pamoja na jengo la nje OPD pamoja na Maabara ambapo mradi huo wa majengo utagharimu kiasi cha shilingi milioni 500. 


Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kakonko Stephano Mag'hanila amesema  kukamilika kwa majengo hayo itakuwa chachu ya ukuaji wa maendeleo ya wilaya hiyo ambapo mradi huo utaongeza uwekezaji mkubwa wa majengo ya kulala  wageni pamoja na kukuza ajira kwa vijana wa wilaya ya Kakonko .


´´ Mradi huu wa hospitali ya wilaya utatoa fursa kwa wakazi wa ndani, wa nje na  wakazi wa wilaya jirani ambapo hospitali  itapokea wagonjwa wa rufaa kutoka nje na hivyo utatoa fursa ya ukuaji wa uchumi wa wilaya kwa  kuwa kutakuwa na uwekezaji wa nyumba za kulala wageni kwa ajili ya watu watakaokuwa wanahudumia wagonjwa wao ´´ alisema  Stephano.



Jengo la OPD katika Hospitali ya Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma inayojengwa katika kijiji cha katika kijiji cha Itumbiko.

Jengo la maabara katika Hospitali ya Wilaya ya Kakonko inayojengwa katika kijiji cha katika kijiji cha Itumbiko.


Post a Comment

0 Comments