Waziri Mkuu wa Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa akiwa akiwa katika mkutano na wananchi wa Butiana mkoani Mara, pembeni ni mama Maria Nyerere. |
Na Mwandishi Wetu
MJUMBE
wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM amesema kati ya wagombea urais
waliojitokeza, hakuna kiongozi zaidi ya Dkt. John Pombe Magufuli.
Alitoa
kauli hiyo siku ya jana (Jumamosi, Septemba 19, 2020) wakati akizungumza na
wakazi wa kijiji cha Butiama, wilayani Butiama, kata za Nyamuswa na Mugeta wilayani
Bunda, akiwa njiani kuelekea Mugumu, Serengeti, mkoani Mara.
“Nimekuja
kuomba kura kwa ajili ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ili
apate miaka mitano mingine kwa sababu hakuna kiongozi bora kati ya wote waliojitokeza
zaidi ya Dkt. John Pombe Magufuli.
“Wanaokuja kuomba uongozi ni wengi lakini hakuna chama chenye benki ya viongozi kama CCM. Hakikisheni mnatupatia viongozi wa CCM ili waweze kufanya kazi pamoja na kwa kuelewana.” alisema.
Aidha
Waziri Majaliwa alitumia mikutanohiyo kumuombea kura mgombea urais kwa
tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, mgombea ubunge wa jimbo la Bunda, Bw.
Boniface Chacha Getere, wagombea udiwani wa wilaya zote mbili za Butiama na
Bunda.
Alisema
uongozi ni lazima utengeneze timu inayofahamiana na inayozungumza lugha moja “Chama
cha Mapinduzi kimeleta viongozi watatu safi. Kwa hiyo ukienda kupiga kura
chagua hao watatu ambao ni mgombea urais, ubunge na udiwani.”
0 Comments