WAZIRI WA KILIMO AWASILI KAGERA KUTATUA KERO ZA WAKULIMA

 

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya ziara ya kikazi  iliyoanza jana tarehe 2 Septemba 2020. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya ziara ya kikazi 

liyoanza jana tarehe 2 Septemba 2020.


Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akisisitiza jambo mbele ya viongozi mbalimbali wa mkoa wa Kagera wakiongonzwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya ziara ya kikazi iliyoanza jana tarehe 2 Septemba 2020.

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera kwa ajili ya ziara ya kikazi 

liyoanza jana tarehe 2 Septemba 2020.



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Kagera

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga jana   Septemba 2, 2020 amewasili Wilayani Bukoba katika mkoa wa Kagera ambapo pamoja na mambo mengine anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Bukoba, Kyerwa, Karagwe na maeneo mengine mahususi yanayojishughulisha na kilimo hususani zao la Kahawa.

 

Lengo la ziara hiyo ni kufuatilia na kujionea hali ya malipo ya wakulima wa kahawa wanaodai, kukutana na viongozi wa vyama vya Ushirika na kufanya mikutano ya kuwasikiliza wananchi kuhusu changamoto zinazowakabili katika sekta ya kilimo.

 

Post a Comment

0 Comments