MILIONI 600 ZATOLEWA KUKAMILISHA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU KIGOMA

Mkurugenzi mkuu wa Ofisi ya Taifa Takwimu (NBS)Dkt Albina Chuwa (kushoto) na Meneja wa Majengo TBA  Mkoa wa Kigoma Julias Chego wakibadirishana nyaraka baada ya kutiliana sahini ya mkataba wa ujenzi wa ofisi ya Takwimu Mkoa wa Kigoma, anaye shuhudia katika ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye.


Na Tryphone Odace,
 Kigoma

Serikali  imetoa  zaidi ya Shilingi Milioni 600 kwa ajili kukamilisha ujenzi wa jengo la  Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoa wa Kigoma, baada ya kukaa kwa zaidi ya miaka 26 bila kukamilika tangu lilipoanza kujengwa mwaka 1994.

 

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu NBS, Dkt Albina Chuwa, alisema hayo wakati wa hafla fupi ya ya kutiliana saini mkataba wa ujenzi wa ofisi hiyo na Wakala wa Majengo nchini TBA.


Kwa upande wake Meneja wa TBA, Mkoa wa Kigoma Julius Daniel, ambao wamepewa miezi miwili tu kukamilisha kazi hiyo, aliahidi kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.


Hafla hiyo ya kutiliana saini ilishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andngenye, ambaye kwa upande wake aliwataka wananchi kutumia takwimu katika ngazi ya familia kwa maendeleo ya familia zao.

 


Post a Comment

0 Comments