Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishina wa Jeshi la Polisi Thobias Andengenye
Na Tryphone Odace
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma Kamishina wa Jeshi la Polisi Thobias Andengenye ameiagiza
polisi kumkamata na kufuta dhamana ya mwanaume anaekadiriwa kuwa
na umria wa miaka 60 anaetuhumiwa
kumlawiti mwanafunzi wa darasa la nne mwenye umri wa
miaka 12.
Alitoa agizo hilo
wakati akizungumza na waandishi wa habari waliomtaka aingilie kati
na kuona namna ya kukomesha vitendo vya ulawiti, ubakaji na matukio mengine ya
ukatili hususani kwa wanawake na watoto ambayo yamekuwa yakiripotiwa bila
hatua kuchukuliwa.
Tukio
la mwanafunzi huyo kulawitiwa lilitokea mwezi Septemba mwaka huu na kuripotiwa
kituo kikuu cha polisi mkoani hapa Octoba 26, huku sababu ya kuchelewa
kuripotiwa ikielezwa kuwa ni baada ya mtuhumiwa kumtishia maisha mwanafunzi
huyo.
Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Alchelaus Mutalemwa amekiri kuripotiwa kwa
tukio hilo na kuahidi kulifanyia kazi agizo la Mkuu wa mkoa haraka
iwezekanavyo.
0 Comments