MZEE MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA MAWE KIGOMA

 




Na Emmanuel Matinde

Mzee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 mkazi wa Mlole kwa jina Jumanne Rashid, amefariki dunia baada ya kuangukiwa na jiwe kubwa wakati akichimba madini ujenzi katika eneo la wachimbaji wadogo wa madini hayo yaliyopo eneo la Masanga Manispaa ya Kigoma Ujiji.

 

Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi Kinga na Tahadhari za Moto katika jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, Sajenti Bahati Salum, kwa niaba ya Kamanda wa Mkoa wa Kigoma wa Jeshi hilo Kamishna Msaidizi Mwandamizi Abdallah Maundu, amethibitisha tukio hilo.

 

“Tulifika eneo la tukio baada ya dakika 15 na tulikuta kweli mwananchi huyo amefukiwa, hatua tuliyoichukua ni kuwasiliana na jeshi la polisi ambao walituruhusu kuchukua mwili na kuupeleka katika hospitali ya mkoa  maweni na hatua zaidi zitachukuliwa pale” alisemaa Sajenti Salumu.

Miongoni mwa walioshuhudia tukio hilo lililotokea jana majira ya saa tisa alasiri ni Hamisi Jonas ambaye pia ni mchimbaji wa madini ujenzi katika eneo hilo la Masanga alisema, “kabla ya tukiwa tulikuwa tunazungumza na yule mzee na baada ya mazungumzo kila mmoja aliendelea na kazi ila baada ya muda tena nilisikia mawe yakidondoka kwa kishindo na nilipoenda kuangalia nikakuta yule mzee ameangukiwa na jiwe

 

Aidha Sajenti Bahati Salum, aliwataka wachimbaji katika eneo hilo wawe waangalifu katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha au wasimamishe kabisa shughuli za uchimbaji hadi pale mvua zitakapomalizika.

 

 

 


Post a Comment

0 Comments