MATOKEO ya uchaguzi wa Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) yamempa ushindi wa kishindo Deogratius Nsokolo ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Kigoma huku akiwa amechukua nafasi hiyo kwa mara nyingine tena.
Nsokolo amepata kura 72 katika kura 83 ziliopigwa na
wajumbe 83 huku mpinzani wake Edwin Soko ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya
Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza akipata kura 11 pekee.
Matokeo hayo yanampa
nafasi Deogratius Nsokolo kutumikia nafasi ya Urais wa UTPC kwa miaka mingine
mitano kuanzia 2020-2025 ambapo awali alitumika katika nafasi hiyo mwaka
2015-2020.
Matokeo kwa ujumla haya
hapa:
Wagombea wanawake
Walioshinda nafasi ya
ujumbe wa bodi ya wakurugenzi UTPC ni
1. Hadija Omar 48
2. Lilian Lucas 51
3. Salma Abdul 62
4. Paulina David 63
Jumla ya kura zilizopigwa
ni 83
Wagombea nafasi za ujumbe
Bodi ya Wakurugenzi UTPCW anaume walioshinda ni
1. Mussa Yusuf 51
2. Cloud Gwandu 61
3. Frank Leonard 64
4. Abdallah Mfaume 69
Kura zilizopigwa ni 83
Kundi la wataalam alikuwa
mgombea mmoja
Eliazer Mafuru kapata kura
zote 83 za ndiyo
Kura za Makamu wa Rais
UTPC
Wagombea ni
1. Lulu George 18
2. Pendo Mwakyembe 65
Kura halali ni 83
Kura za Rais wa UTPC
1. Deo Nsokolo 72
2. Edwin Soko 11
Kura halali 83
0 Comments