Tanzania na Burundi waendelea kuimalisha mahusiano ya kibiashara.

 

Mkuu wa wilaya ya Kibondo bw. Luis Bura (picha na James Jovin )


KIBONDO

Mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Burundi yanaendelea kuimalishwa ambapo soko la kimataifa lililojengwa katika kijiji cha Mkalazi wilayani Kibondo litaanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu likihusisha wafanyabiashara wa nchi za Burundi na Tanzania

 

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya Kibondo bw. Deocres Rutema wakati wa ziara ya pamoja na viongozi wa mkoa wa Ruyigi nchini Burundi katika eneo ambalo limejengwa soko hilo

 

Bw. Rutema amesema kuwa soko hilo litasaidia  kukuza uchumi wa nchi zote mbili lakini pia litasaidia kwa kiasi kikubwa kuendeleza mahusiano mema na kuimalisha ulinzi na usalama kwa kiasi kikubwa

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara wilaya ya Kibondo bw. Plan Nzuguru amesema kuwa mahusiano kati ya Tanzania na Burundi yataleta mabadiliko chanya katika sekta ya uchumi

 

Aidha  mkuu wa mkoa wa Ruyigi nchini Burundi bi. Tabu Emeransiene amepongeza hatua kubwa iliyofanywa kwa upande wa Tanzania na kwamba atapeleka ujumbe kwa viongozi wake ili waweze kuanza ujenzi kwa upande wa Burundi kwa kuwa miradi hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa pande zote mbili.

 

Mkuu wa wilaya ya Kibondo bw. Luis Bura ameshukuru kwa ugeni huo kutoka nchi jirani ya Burundi na kwamba mahusiano mazuri yamekuwa yakisaidia hata kutatua changamoto mbali mbali zikiwemo za ulinzi na usalama

 


Post a Comment

0 Comments