Na Emmanuel Matinde, Kigoma
Imeelezwa kuwa
ukosefu wa mitaji, uoga wa kuthubutu ni miongoni mwa vikwazo kwa wajasiriamali
wanawake wa mkoa wa Kigoma kushindana katika zabuni mbali mbali zinazotolewa
serikalini.
Hayo yalielezwa
na baadhi ya wanawake wajasiriamali wa mkoa wa Kigoma, katika mahojiano na Blog
hii, ambapo pia walisema changamoto nyingine ni upatikanaji wa taarifa, ukosefu
wa elimu na uelewa kuhusu zabuni zinazotolewa na serikali.
“Serikali kweli
sasahivi imeamua kutoa kipaumbele kwa wanawake kutoa mitaji lakini kusema ukweli mitaji bado
haijawafikia wale wajasiliamali haswa ambao biashara zao ni kubeba mabeseni ya
mihogo, viazi na karanga ambao hao ndio
walikuwa wanalengwa na serikali, lakini pesa hizo zinaenda kwa wale ambao
wanajiweza kifedha
Aidha Afisa
Manunuzi na Ugavi wa Mkoa wa Kigoma, Baraka Baligumya, alisema kwa kutumia
mashirika yasiyo ya kiserikali wanawake wanaendelea kupatiwa elimu ili waweze
kupata uelewa wa kutosha na hatimaye kuwania fursa za zabuni serikalini, pia
akibainisha kuwa kundi la wanawake ni moja ya makundi maalum ambayo sheria inawapa
fursa ya kuchukua zabuni za serikali.
“Kutokana na sheria
ya manunuzi namba 9 ya mwaka 2013 imewapa upendeleo watu wa kutoka makundi
maalumu wakiwemo wanawake ikiwa ni upendeleo wa 30% na kwa katika kila tenda
zinazojitokeza 30% wawe ni watu wanaotoka katika makundi maaluamu hasa wanawake”
alisema Baligumya.
Kwa mujibu wa
Afisa Manunuzi na Ugavi wa Mkoa wa Kigoma, hali ya wanawake kujitokeza katika
zabuni za serikali iko chini ya wastani na moja ya sababu ni kutosajili
vikundi.
0 Comments