WAJASILIAMALI KIGOMA WATAKIWA KUTUMIA TAASISI ZA KIFEDHA KUJIINUA KIUCHUMI

Na Mwajabu Kigaza, Kigoma

Wajasiliamali mkoa wa Kigoma wametakiwa kutumia taasisi za kifedha ili waweze kupata taarifa mbalimbali zitakazowawezesha kuendeleza biashara zao na kusaidia kuinua uchumi wa kipato chao.

Kauli hiyo ilitolewa na meneja kanda ya magharibi Said Pamui kutoka banki ya CRDB  wakati wa semina elekezi ya mpango maalumu kwa wanawake wajasiliamali mpango ambao utachochea maendeleo yao kwa kutumia fusra za kiuchumi zilizopo mkoani Kigoma.

Viongozi wa Bank ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja na wajasilimali wa wilaya za Buhigwe na Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma

“Hii ni dhana ambayo itachangia kwa kiasi fulani kuunga mkono juhudi za serikali kuwaletea maendeleo wananchi hususani wanawake, banki ya CRDB inaamini kwamba kumjuza na kumuelekeza mwanamke katika fani mbalimbali za ujasiliamali itakuwa imefanikiwa kuliendeleza Taifa kwa kiwango kikubwa kiuchumi”

Mkuu wa kitengo cha uwezeshaji wanawake kiuchumi CRDB Rachel Senni amesema lengo ni kumuinua mwanamke kiuchumi kwa kumpatia elimu ya kupata mikopo, kutunza akiba pamoja na kufahamu namna ya kutunza kumbukumbu ambapo akaunti ya malkia imeelezwa kuwa suluhisho la changamoto kwa wajasiliamali wanawake.

Meneja wa bank ya CRDB kanda ya magharibi Said Pamui, akizungumza wakati wa semina ya wajasiliamali wa wilaya za Buhigwe na Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma.

Malkia ni akaunti ya malengo ambapo inatumika kuweka fedha kwa kipindi cha mwaka mzima na unakuwa na malengo ambapo kila siku katika hela ya faida unatoa 1700 mpaka mwezi unaisha unakuwa na kiasi cha shilingi elfu 51,000/= ambapo kwa mwaka unakuwa na hela ya kutosha lakini pia unaweza kuitumia kuchukulia mkopo banki” alisema.

Semina hiyo ambayo iliwakutanisha wajasiliamali wanawake kwa nyakati tofauti katika  wilaya ya Buhigwe pamoja na Manispaa ya Kigoma Ujiji imekuwa na manufaa makubwa ambapo baadhi ya wajasiliamali walieleza jinsi ambavyo mpango huo utakuwa na msaada kwao ikiwemo kuepukana na changamoto ya ukosefu wa mitaji, utunzani wa kumbukumbu na utafutaji wa masoko.

Mkuu wa kitengo cha uwezeshaji wanawake kiuchumi CRDB Rachel Senni akitoa semina kwa wajasiliamali wilaya za Buhigwe na Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma.


 

Post a Comment

0 Comments