WANANCHI WALALAMIKIA KUTORIDHISHWA NA FIDIA YA KUBOMOLEWA MAKABURI KIGOMA

Gari aina ya Greda likiendelea kuhamisha makaburi eneo la ujiji Manispaa ya Kigoma Ujiji kwaajili ya kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege mkoani Kigoma.


Na Isaac Aron Isaac, Kigoma

Wananchi wa eneo la Ujiji, Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma ambao wamebomolewa makaburi yao wameeleza kutoridhishwa na utaratibu unaotumiwa na serikali katika ulipaji wa fidia ya makaburi hayo  kwaajili ya upanuzi wa uwanja wa Ndege wa mkoa huo.

Wakizungumza na Blog hii baadhi ya wananchi ambao makaburi yao yamevunjwa kwaajili ya kupisha upanuzi wa uwanja walisema utaratibu wa kila mtu kusimama juu ya kaburi ili kulipwa fidia haujatenda haki kulinga na mazingira ya eneo hilo.   

Baadhi ya wananchi wa eneo la Ujiji, Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma wakiwa wamesimama kwenye makaburi kwaajili kulipwa fidia kabla ya kuhamishwa kwa makaburi hayo.
                   

“Malalamiko yetu ni baada ya kupewa idadi ndogo ya makaburi kinyume na hali halisi, cha ajabu wengine hawajalipwa kabisa licha ya kuwa wana makaburi halafu watu wengine hawako kwenye utaratibu lakini walilipwa” walisema.

Aidha baadhi ya wananchi walikubaliana na hatua ya serikali “Kuliko kukosa vyote ni kheri kupata kidogo kilichopo kwani kukataa zoezi la kubomoa makaburi haliwezi saidia chochote sisi watupatie hizo pesa lakini na wengine hawana budi kukubaliana na hali ili wakawahifadhi ndugu zao sehemu nyingine”  Walisema.

 

Ngege ya shirika la Ndege Tanzania ikiwa katika uwanja wa ndege wa Kigoma ambao unatarajiwa kufanyiwa malekebisho ya kupanuliwa.

Hata hivyo Uamuzi wa serikali ukawa ni  kuendelea na zoezi hilo licha ya uwepo wa mgomo kwa baadhi ya wananchi ambapo Meneja  wa Tanroad mkoa wa kigoma Mhandisi Narsisi Choma amesema zoezi hilo la kubomoa makaburi  linaweza chukua siku mbili kisha taratibu nyingine kufuatwa ikiwemo kumpata mkandarasi ili ujenzi wa upanuzi uanze mara moja

Upanuzi wa Uwanja wa Kigoma ni moja kati ya hatua ambayo serikali inachukuwa ikiwa ni sehemu ya kuboresha usafiri wa anga kwani karibu asilimia 40 ya wasafiri wanaotumia uwanja huo hutokea nchi jirani soko ambalo serikali inalenga  kuliboresha Zaidi.


Post a Comment

0 Comments