WANANCHI WATAKIWA KUHESHIMU NA KULINDA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA BURUNDI

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishina wa jeshi la polisi Tibias Andengenye wa pili kutoka kushoto akiwa na baadhi ya viongozi kutoka nchini Burundi wakati wa kikao cha maazimio ya ujirani mwema.

Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Wananchi wa nchi za Tanaznia na Burundi wametakiwa kuheshimu makubaliano ya amani na ushirikiano baina ya nchi hizo kama viongozi wa nchi hizo walivyo kubaliana kuwa na ushirikiano na kukomesha matukio ya ujambazi kwa lengo la kuwa na usalama katika pande zote.


Hayo yalizungumzwa na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina wa jeshi la polisi Thobias Andengenye katika mkutano wa maazimio ya mkutano wa ujirani mwema kati ya mkoa wa Kigoma na mikoa mitaano ya Burundi ambayo ni Makamba, Rutana Ruyigi, Cankuzo na Rumonge.


“Tangu kuanzishwa kwa ushirikiano baina ya nchini hizi mbili mwaka 2004 kumekuwa na manufaa ambapo kumekuwa na kasi kubwa ya kutengeneza mazingira wezeshi ili kuendana na kile ambacho viongozi wa nchi hizi waliadhimia kuendeleza ushirikiano ili wananchi waweze kunufaika na rasilimali zilizopo katika nchi zao” alisema Kamishina Andengenye.

 

Nae Mkuu wa Mkoa wa Makamba nchini Burundi Bi Francoise Ngozirazana alisema wataendelea kushirikiana na Tanzania kwani tangu kuanzishwa kwa ujirani mwema matukio ya uhalifu yamepungua.

 

“Kigoma imetusaidia sana kutokana na cnhi ya Burundi kuwa katika vita kwa miaka mingi, naishukuru sana Tanzania kwa kusimama na kutusaidia kupambana na majambazi waliokuwa wakitaka kuja kuikosesha amani Burundi” alisema Ngozirazana.

 

Hata hivyo baadhi ya wajumbe waliohudhuria kwenye mkutano huo akiwemo Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia General Marco Gaguti pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homela walisema hali ya usalama ni shwari licha ya kuwepo matukio kadhaa ambayo wamefanikiwa kupambana nayo.

 


Post a Comment

0 Comments