Na Kadisilaus Ezekiel.
Wanawake wanaojifungua katika kituo cha afya Kigamano katika
Halmashauri ya mji wa Kasulu mkoani Kigoma wameiomba serikali kuongeza
miundombinu ya afya ya uzazi ikiwemo majengo na vitanda kufuatia ongezeko la
wanawake wanaojifungulia kituoni hapo na kupelekea kitanda kimoja kutumiwa na
wanawake wawili hadi watatu.
Wakizungumza mara baada ya kutembelewa na mbunge jimbo la
Kasulu mjini Prof. Joyce Ndalichako baadhi ya wanawake hao akiwemo Anita Shedrack
na Salome Samwely walisema wanahitaji huduma ziboreshwe kituoni hapo sambamba
na kupewa elimu ya uzazi ili waweze kuwa salama wao na watoto.
Mbunge wa jimbo la Kasulu Mji Prof Joyce Ndalichako akizungumza na akina mama alipotembelea kituo cha afya cha Kiganamo kilichopo halmashauri ya Kasulu Mji mkoani Kigoma. |
“Hatua hiyo pia hutokana na huduma bora zinazotolewa na wahudumu, na tutaendelea kutoa huduma bora kwa akina mama ili kulinda afya zao na watoto wao” alisema.
Mbunge wa jimbo la Kasulu Mji Prof Joyce Ndalichako akiwa amebeba mtoto baada ya kutembelea wodi ya wazazi katika kituo cha afya cha Kiganamo kilichopo halmashauri ya Kasulu Mji mkoani Kigoma. |
“Mpango uliopo ni kurekebisha majengo
yasiyotumika ili nayo aanze kutoa huduma jambo litakalotoa nafuu kwa wananchi
wanaotumiaa kituo kimoja cha afya” alisema Bi. Fatma.
Naye Mbunge jimbo la Kasulu Mjini Prof. Joyce Ndalichako
alieleza kuzifikisha changamoto zinazowakabili wananchi wa jimbo lake hasa
ukosefu wa vituo vya afya kwa serikali kuu ili ziweze kupatiwa
ufumbuzi na kwamba kata nyingine zitegemee kupata vituo vya afya kama ambavyo
ilani ya ccm inavyoeleza katika kuwahudumia wananchi.
0 Comments