WILAYA YA KIBONDO YAANZISHA KILIMO CHA ZAO LA KOROSHO


 

KIBONDO

 

Halimashauri ya wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imeanza mkakati wa kilimo cha korosho ambapo tayari wakulima wamesaidiwa kuanzisha zaidi ya ekali 1800 mpaka sasa na kupewa elimu ya zao hilo ili kuanzisha kilimo cha biashara kitakachowakomboa kiuchumi na taifa kwa ujumla

 

Hayo yamebainishwa na mratibu wa zao la korosho katika wilaya ya Kibondo bw. Victor Kabunga wakati wa semina elekezi kwa maafisa ugani na wakulima wa zao hilo  juu ya utambuzi wa magonjwa na wadudu waharibifu wa zao la korosho

 

Aidha bw. Kabunga amesema kuwa halimashauri ya wilaya ya Kibondo ilianza rasmi kilimo cha korosho mwaka 2019 ambapo imekuwa ikitoa elimu kwa wakulima juu ya zao hilo na kuwapa mbegu bila malipo ili waweze kulima zao hilo litakalowakwamua kiuchumi

 

Kwa upande wao baadhi ya wananchi na wakulima wa wilaya ya Kibondo wameonekana kuchangamkia fursa hiyo na kuanza kulima zao la korosho hata hivyo wameitaka serikali kuwawekea mazingira mazuri na kuwahakikishia soko la uhakika

 

Nae afisa kilimo kutoka bodi ya korosho Tanzania bw. Mandela Chikawe amewahakikishia wakulima wa zao hilo katika wilaya ya Kibondo kuwa iwapo watalima kwa tija zao hilo kufikia mwaka 2014 linaweza kuingiza zaidi ya bilioni 7 hivyo kujikwamua kiuchumi na serikali kwa ujumla. ENDS


Post a Comment

0 Comments