KIBONDO
Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Kumsenga iliyoko wilayani Kibondo anayekadiliwa kuwa na miaka 15 ametorokea kusikojulikana baada ya kupewa ujauzito na kijana wa rika lake ambaye si mwanafunzi
Akizungumza na KGPC Blog afisa mtendaji wa kijiji cha Kukinama kata ya Kumsenga bw. Mpaji
Juma amesema kuwa mwanafunzi huyo wa darasa la tano pamoja na kijana aliyempa
mimba wametoroka wote kwa pamoja ikiwa ni masaa machache baada ya kupewa wito
wa kufika ofisi za kijiji wao pamoja na wazazi wao
Aidha amesema
kuwa mwanafunzi huyo alikuwa tayari ameacha shule zaidi ya miezi miwili
iliyopita na inaonekana wazazi wa pande zote mbili huenda wanahusika na
walikuwa katika mpango wa kuwaozesha vijana wao kwa kuwa licha ya kumuona
kijana wao akiwa na mimba lakini hawakutoa taarifa popote
Baada ya
watoto hao kutoroka wazazi wa pande zote mbili wamekamatwa na kufikishwa kituo
kidogo cha polisi kumsenga ili waweze kuwajibishwa kwa kuwa inaonekana
wamehusika kwa namna moja ama nyingine katika tukio hilo lililopelekea
mwanafunzi huyo wa darasa la tano kupoteza ndoto zake. ENDS
0 Comments