SEKTA YA AFYA KIGOMA YAFANIKIWA KUKABILIANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO


Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Sekta ya Afya mkoani Kigoma imeeleza katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2018 imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu ambacho kilikuwa kikiathiri eneo kubwa la mkoa huo.

Mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma Dkt Saimon Chacha alieleza hayo wakati wa makabidhiano ya vifaa kwaajili ya wahudumu wa afya kutoka taasisi ya Benjamini Mkapa vilivyo na thamani ya million 74 kwa lengo la kusaidia kuwakinga watoa huduma na magonjwa mbalimbali ya mlipuko.

Ni miaka mitatu ya jitihada kubwa kwa sekta ya afya mkoani Kigoma ambayo iliongeza kasi baada ya kuingia kwa maambukizi ya Covid 19 ambapo wagonjwa sita pekee walipata maambukizi hayo, lakini kipindupindu imekuwa kadhia ya muda marefu kwa wakazi wa mkoa huu.

 Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishina wa Jeshi la Polisi Tobias Andengenye wa kwanza kushoto akipokea sehemu ya msaada wa vifaa vitakavyotumiwa na watoa huduma kujikinga na magonjwa ya maambukizi, anaye mkabidhi ni Zawadi Dakika afisa miradi taasisi ya Benjamini mkapa. 


Mganga mkuu wa Mkoani wa Kigoma Dkt Saimo Chacha alisema miaka mitatu ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko imeanza kuzaa matunda, tayari kwa asilimia kubwa uthibiti wa magonjwa hayo ambayo yaliathiri hasa wilaya ya Uvinza na kambi za wakimbizi inaendelea kushika kasi kuhakikisha wananchi wanabaki salama.

Jitihada hizo zinachagizwa na wadau wa maendeleo ambao nao wanaona ipo haja ya kuimarisha idadi ya watoa huduma za afya ambao kwa mkoa wa Kigoma bado ni ndogo ambapo taasisi ya Benjamini Mkapa imefanikiwa kuajiri watia huduma 197 katika vituo vya afya mkoani hapa sambamba na utoaji wa vifaa vya kujikinga na magonjwa ya maambukizi katika halmashuri zote nane.

Sehemu ya vifaa vilivyotolewa na taasisi ya Benjamini Mkapa kwaajili ya kwaajili ya wahudumu 

Mchango wa wadau wa maendeleo katika sekta ya afya kwanza kabisa ukapongezwa na mkuu wa mkoa wa kigoma Thobias Andengeye kisha kibao kikageukia kwa watumishi wa afya ambao ndio wako mstari wa mbele kuhakikisha hali ya kiafya mkoani hapa inazidi kuimarika kuhakikisha wanatumia taaluma yao vyema kulinda mkoa wa Kigoma.

Post a Comment

0 Comments