KIBONDO
Watu watatu
wakazi wa kijiji cha Kigina kata ya Rugongwe wanashikiliwa na serikali ya
kijiji hicho kwa tuhuma ya kujihusisha na biashara haramu ya kuuza nyama za
Mbwa kinyume na maadili ya kitanzania
Akizungumza na KGPC Blog afisa mtendaji wa kijiji hicho bw. Shedrack Totoye amewataja watuhumiwa
hao kuwa ni Bahati Ngubaguba, Lucas
Shija pamoja na Ndikumana Paul wote wakazi wa kijiji cha Kigina
Aidh bw.
Shedrack amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa hapo jana January 11 katika
soko la Kitongoji cha Malimbi kijiji cha Kigina ambapo wamekuwa wakichanganya
nyama ya mbwa pamoja na mbuzi au Nguruwe na kuwauzia wananchi kwa masirahi yao
binafsi
Mmoja wa
watuhumiwa hao bw. Bahati Ngubaguba akizungumza na redio kwizera amekili
kujihusisha na biashara hiyo ambapo amesema kuwa amekuwa akiwauzia wananchi
wanaopenda nyama hiyo ambapo pia yeye mwenyewe amekuwa akiitumia kama kitoweo,
Tayari watuhumiwa wote wamefikishwa kituo kidogo cha polisi Rugongwe kwa
mahojiano zaidi. ENDS
0 Comments