Hatimaye Mhandisi Atashasta Nditiye amezikwa kijijini kwao Kumwambu


 

KIBONDO

 

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la muhambwe wilayani Kibondo mkoani Kigoma amezikwa leo kijijini kwao Kumwambu kufuatia ajali aliyoipata February 10 eneo la nane nane jijini Dodoma na kufariki dunia February 13 wakati akipatiwa matibabu.

 

Mazishi hayo yamehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali akiwemo waziri mkuu wa Tanzania Majaliwa kasimu, Naibu sipika Tulia akisoni, waziri wa elimu profesa Joyce Ndalichako aliyewakilisha wabunge wa mkoa wa Kigoma

 

Waziri mkuu kasimu Majaliwa akitoa salamu za rambi rambi amesema kuwa marehemu Atashasta Nditiye wakati wa uhai wake alifanya kazi kwa uadilifu mkubwa  na kuwatumikia wananchi kwa upendo hivyo pengo lake ni kubwa katika jamii na familia yake kwa ujumla

 

Kwa upande wake waziri wa Elimu profesa Joyce Ndarichako pamoja na naibu spika Tulia Akisoni wakitoa salamu zao za rambi rambi wamesema kuwa marehemu Atashasta Nditiye ni moja kati ya wabunge ambao walijitolea sana kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya taifa na jamii kwa ujumla.

 

Baadhi ya wananchi wanaoishi katika jimbo la Muhambwe wamepokea kifo cha mbunge wao kwa masikitiko makubwa kwa kuwa alikuwa mbunge mwenye mipango mingi ya maendeleo

 

Misa ya mazishi na kumuaga marehemu imefanyika katika kanisa Anglikana la mtakatifu Hilario kanisa kuu la dayosisi ya Kibondo misa ikiongozwa na baba askofu Sospiter Temeo Ndenza

 

Marehemu Nditiye amefariki kwa ajali ya gari akiwa na umri wa miaka 52 ambapo ameacha mke na watoto watatu katika kipindi hiki ambapo alikuwa amechaguliwa kulitumikia jimbo la muhambwe kwa awamu ya pili, bwana alitoa bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe.

 


Post a Comment

0 Comments