CHANGAMOTO BADO ZINAWAKABILI WANAWAKE


Na Adela Madyane, Kigoma

Licha ya ukuaji wa tasnia ya habari nchini wanawake bado wanakabiliwa na Changamoto nyingi kwani nafasi nyingi za uongozi zinasimamiwa na wanaume na si wanawake.

Changamoto kubwa ambayo  wanawake wameendelea kukabiliana nayo ni umiliki wa vyombo vya habari kwani vingi humilikiwa na wanaume hivyo huwapa nguvu wanaume wenzao na wanawake kubaki kama waandishi wa habari na si kama wahariri au mameneja. Japo wapo wanawake wahariri lakini bado kuna namna ya kufanya kwaajili ya kuongeza idadi yao

Na hii ndio sababu hasa inakuwa ngumu kushinikiza na kujumuisha  masuala ya usawa wa kijinsia kwasababu wanawake wengi hawapo karibu na chombo Cha kufanya maamuzi

Tunaposherehekea siku ya wanawake duniani yenye kichwa "wanawake  katika uongozi katika ulimwengu wa COVID-19 kuna haja wanawake wakavaa vazi katika nafasi za juu za uongozi , wanawake hawapaswi kuogopa kutafuta fursa za ukuaji katika taaluma yao

Katika kipindi hiki Cha COVID-19, wanawake na wanaume hodari katika tasnia ya habari wamekuwa wakiendelea kufanya kazi vizuri katika kutoa habari muhimu kwa umma jambo ambalo linapaswa kuhimizwa na kupongezwa vilivyo.

Hivyo kutokana na juhudi hizo itapendeza kwamba sera za vyombo vya habari kuendelea kuhimiza  na kulazimisha wamiliki wa  vyombo vya habari kuteua asilimia fulani ya wanawake katika nafasi za juu ya kufanya maamuzi, itapendeza ikiwa 50/50 au 50/60 kutokana na wanawake kuwa wengi kiidadi

Na kwa wanawake ambao tayari ni wahariri na wanashika nyadhifa mbalimbali katika vyombo vya habari wanapaswa kuacha kuharibu mitazamo ambayo inaharibu taswira ya mwanamke lakini badala yake wawawezeshe wanawake wenzao kuchukua nyadhifa  pia Ili kuinua taaluma yao, familia zao na taifa kwa ujumla.  

 


Post a Comment

0 Comments