Na Mwandishi Wetu Kasulu, Kigoma
Mkuu wa wilaya ya
Kasulu Mkoani Kigoma, Kanal Saimon Anange ameiomba serikali kupitisha sheria ya
adhabu kwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakiwa shuleni ili kusaidia
kupambana na changamoto hiyo.
Kanal Anange amesema hayo
katika hafla iliyowakutanisha wadau wa elimu, waalimu na wanafunzi ambapo
amesema sheria iliyopo kwa sasa ya kifungo cha miaka 30 jela inapaswa kutumika
kwa wote wawili pale wanapokutwa na hatia.
Baadhi ya wanafunzi wa
Shule za Msingi na Sekondari hapa Mkoani Kigoma wamesema endepo sheria hiyo
ikifanyiwa marekebisho itakuwa na tija
katika kupambana na mimba mashuleni.
0 Comments