Na Mwandishi Wetu
Waziri Mkuu wa
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amewataka Watanzania kupuuza
taarifa za upotoshaji zinazotolewa mitandaoni juu ya Afya ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
Waziri Mkuu
amesema hayo hii leo March 12 Mkoani Njombe mara baada ya kushiriki swala ya
Ijumaa katika Msikiti wa Wilaya ya Njombe ambapo amewataka
watanzania kuwa watulivu kwani Rais Magufuli yupo salama na anaendelea na
majukumu yake.
Aidha amewataka watanzania
kuendelea kuliombea Taifa, huku viongozi wakitakiwa kukemea roho za
chuki na kuhimiza upendo miongoni mwa watanzania.
0 Comments