WAZIRI NDALICHAKO AAGIZA MKUU WA CHUO CHA VETA KIGOMA AVULIWE MADARAKA

 


Na Isaac Aron, Kigoma

Waziri wa elimu Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako ameagiza kuvuliwa madaraka kwa mkuu wa chuo cha ufundi stadi veta mkoani Kigoma kutokana na kushindwa kusimamia vyema ujenzi wa chuo cha Veta Wilayani Buhigwe mkoani humo.

Ndalichako alitoa maagizo hayo katika ziara yake ya kutembelea ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi Veta katika wiaya za Uvinza,Kasulu na Buhigwe vinavyojengwa chini ya mpango wa serikali wa kujenga vyuo 25 nchi nzima kwa gharama ya shilingi billion 40 katika awamu ya kwanza.

Ujenzi wa chuo cha ufundi stadi Veta wilayani Buhigwe ambao unajengwa na chuo cha veta mkoani kigoma unatarajiwa kugharimu shilingi billion 1.6 kwa ujenzi wa majengo 17 ambayo yanatakiwa kukamilika mwisho mwa mwezi june mwaka huu.

Waziri wa elimu Prof Joyce Ndakichako anatembelea mradi huo na kuonyesha kutiridhishwa na ujenzi wake kutokana na kujengwa chini ya kiwango cha serikali na kumlazimu kutoa maagizo kwa mkurugenzi wa Veta nchini.

Mkurugenzi mkuu wa Veta Dkt Pancras Bujulu alieleza kupokea maagizo hayo na kufanyia marekebisho katika mradi huo ili kufikia mwezi june wananchi waanze kupata huduma katika chuo hicho.

Baadhi ya wakazi kutoka wiliya za Buhigwe Uvinza na Kasulu waliishukuru serikali kwa ujenzi wa vyuo hivyo utakaosaidia jamii zao kujiendeleza kiuchumi kupitia elimu za stadi ya maisha watakayopata katika vyuo hivyo.

Katika hatua nyingine Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako alitoa maelekezo kwa vyuo vyote vya veta ambavyo vimepewa dhama ya ujenzi wa vyuo vipya vya ufundi stadi kuhakikisha wanakamilisha miradi hiyo kwa wakati ifikapo mwezi june mwaka huu.

 

Post a Comment

0 Comments