KASI YA MAGONJWA YA MLIPUKO YAPUNGUA TANZANIA

Mkurugenzi wa NEMC, Dk. Samuel Gwamaka,

 

Na Mwandishi Wetu,

Magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu imetajwa kuwa tishio kwa maendeleo ya ustawi wa jamii na uchumi wa mataifa mengi Barani Afrika hasa yaliyopo Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania ikiwamo.

Aidha, pamoja na magonjwa hayo, nchi zilizopo katika ukanda huo zinakabiliwa pia na majanga mengine ya kiasili kama vile ukame, mafuriko na migogoro jambo ambalo linapelekea magonjwa ya mlipuko kuathili zaidi wananchi wa maeneo hayo

Nchi ya Tanzania kwa muda mrefu sasa imekuwa ikiendelea kupambana na magonjwa ya mlipuko huku magonjwa ambayo yamekuwa yakisumbua wananchi katika maeneo mbalimbali nchini yakiwa ni pamoja na Kipindupindu

Wakati mapambano hayo yakiendelea Imelezwa kuwa Tanzania imefikia hali ya kupungua kwa kasi ya magonjwa ya mlipuko hususan kipindupindu hapa nchini ndani ya miaka 5.

Hayo yalielezwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambapo limesema, kupungua huko kumetokana  na usimamiaji mzuri wa sheria na kanuni za mazingira.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa NEMC, Dk. Samuel Gwamaka, alisema kuwa utoaji wa elimu hasa katika kipindi cha awamu ya tano ni moja ya sababu, pia amewapongeza  Watanzania kwa  kuweka mazingira safi na salama bila shuruti.

Dk. Gwamaka aliongeza kwamba chanzo kikubwa cha magonjwa ya milipuko nchini ni utiririshaji wa maji taka katika maeneo ya makazi ya watu pamoja na maji ya kemikali zenye sumu kutoka viwandani ambayo huelekezwa katika mito na makazi ya watu.

 Hata hivyo Dkt Gwamaka alisema kuwa kutokana na mwitiko chanya wa wananchi, NEMC imeunda kikosi kazi cha dharura ambacho kinafanya kazi saa 24 huku kazi yake ikiwa ni kuhakikisha changamoto za kimazingira zinashughulikiwa kwa wakati.

 


Post a Comment

0 Comments