WAANDISHI WA HABARI NCHINI KUNUFAIKA NA MNGO WA BIMA YA AFYA

 


Muungano wa klabu za waandishi wa habari Tanzania UTPC kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa bima ya afya NHIF umezindua mpango wa utoaji bima ya afya kwa waandishi wa habari nchini baada ya UTPC kufanya mazungumzo na NHIF kukubali waandishi kuwa na kifurushi chao maalum.

 

Akifungua mpango huo, mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amewataka waandishi wa habari kuacha ubahili na kulipia fedha hizo ili kuwa na uhakika wa matibabu wanapougua.

 


Nae Rais wa UTPC Deogratius Nsokolo  ameushukuru mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF kwa kujali afya za waandishi wa habari huku akiwashukuru pia waandishi wa habari nchini nzima kwa kuomba wawetengewe kifurushi chao maalumu.

 

“Asante Press club zote nchini ambazo wakati maafisa wa NHIF wanapita kuhamasisha mikoani waandishi walipaza sauti kuanzia Mtwara hadi Kagera kuomba kifurushi maalum na UTPC kufanya coordination na hatimaye sasa mpango umeanza rasmi” alisema Rais wa UTPC

 

Rais wa UTPC Deogratius Nsokolo

Rais Deogratius amebainisha kuwa hadi sasa mkoa wa Kigoma licha ya kuwa na wanachama wachache ndo inaongoza kwa waandishi kuwa na bima ya afya.

 

Ameongeza kuwa wanachama wa press clubs nchini wanakaribia 1800 lakini mpango huu  umezinduliwa ukiwa na wandishi 80 pekee

 


Hata hivyo Rais Deogratius ametoa wito kwa kwa waandishi wote hata wale wasio wanachama wa press club  kujiunga na mpango huo kupitia press club katika mikoa yao.

 


 


 


 

 

Post a Comment

0 Comments