Adela Madyane, Kigoma
Wananchi
wanaoishi mwambao mwa ziwa Tanganyika pamoja na ofisi mbali mbali zilizopo
pembezoni mwa ziwa Tanganyika eneo la Kibiri Mkoani Kigoma wamekubwa na
athari za kimazingira kutokana na ongezeko la maji katika ziwa hilo tangu
April mwaka 2021.
Kwa
mujibu wa Muhandisi kutoka bodi ya maji Bonde la ziwa Tanganyika
Respicious Mshogozi alisema chanzo cha athali hiyo ni maji kushuka toka mwaka
1974 na kuanza kupanda mwaka 2006 ambapo takwimu ya chini kusomwa ilikuwa772.85
ambayo ni sawa na ongezeko la nusu mita kutoka kwenye usawa
wa ziwa toka mwaka 2006.
Mshogozi
alisema maji yalianza kuongezeka na hadi kufikia April mwaka 2012 kina
cha maji kilipanda na kusoma776.42 kutoka wa ziwani .
Takwimu
hizo zimeendelea kubaki kuwa 776.47 kwa mwezi May 202. Wastani wa ziwa ni sawa
na 772.35 hivyo kuleta ongezeko la sentimeta 4.12 kutoka wastani wake.
Mshogozi
ameongeza kuwa maji yataanza kupungua kunzia mwishoni mwa mwezi wa 6 kuelekeza
wa 7, na yapungua zaidi kuanzia mwezi wa 9 na wa 10,na yataanza kuongezeka
zaidi kuanzia Novemba 2021 ambapo mvua zinatarajia kuanza kunyesha.
David
Manyama Kaimu Mkurugenzi wa bonde la maji Ziwa Tanganyika, alisema kuwa
maziwa yakijaa hupungua taratibu, na zipo sasababu kuu mbili za asili
zinazopunguza maji ambazo ni maji kuvukizwa, mvuke kupanda angani na maji
kutoka kwenye njia yake ya asili.
“maji
ya ziwa Tanganyika yanatoka kwenda ziwa Atlantiki kupitia mto Lukuga
uliopo Kalemi nchini Kongo, mto Lukuga hupeleka maji yake katika mto mwingine
mkubwa zaidi ambao huo huingiza maji mto Kongo na kisha kuingia kwenye bahari
ya Atlantiki ” Alisema Manyama.
Sababu
nyingine ndogo za kupunguza maji ziwani kwa kiasi kidogo ni matumizi ya
shughuli za kibinadamu zinazohusisha kilimo cha umwagiliaji na matumizi ya
nyumbani.
Vipo
vyanzo na njia mbalimbali zinazoogeza maji ziwani zikiwemo mvua,
mitoinayotiririsha maji ziwani, na maji chini ya ardhi, kuna mikondo
inayoingiza maji ziwani, uwiaono wa maji unaoingia na kutoka ziwani ndio
unaosabababisha maji kupungua au kuongezeka.
Maji
yanayotoka yakiwa mengi kuliko yanayoingia husababisha kupungua kwa maji, huku
maji yanayoingia yakiwa mengi kuliko yanayotoka maji huongezeka kulingana na
mabadiliko ndani ya mwaka mmoja ambapo maji hujaa na kupungua.
“
tumeshuhudia ongezeko la maji kuongezeka toka mwaka 2006 lakini zaidi kwa miaka
ya 2019 mpaka sasa, hii inamanisha kuwa maji yanayotoka ni machache kuliko maji
yanayoingia” alieleza Manyama.
Maji
kuongezeka huchukua miaka 15-30 na kupungua huchukua pia miaka 15-30, hivyo
kuna mzunguko wa miaka 60 ya maji kuongezeka na kupungua na kitendo hicho
hutendeka taratibu, ushuhuda wake ni mdogo kwa kuwa tabia hiyo
haijitokezi kwa kasi.
Hata
hivyo vitendo hivyo hufanyika kwa maziwa yote duniani na hasa maziwa
yaliyopo Africa, na kwa kipindi hiki maziwa yote ya Afrika yamejaa, hata yale
yaliyokuwa kwenye hatari ya kukauka huku akitoa mfano wa ziwa Chad, Turkana
pamoja na Natron.
Bakari
Mwichande kaimu mkuu wa kampasi ya Kigoma katika chuo cha Elimu ya afunzo
ya uvuvi (FETA) akielezea namna gani ogezeko la maji limeathiri mazao ya ziwani
ikiwemo samaki na dagaa.
Mwichande
alisema ongezeko la maji ni faida kwa samaki na dagaa kwa kuwa maji
yakiongezeka wanapata maeneo mapya ya kuishi na vilevile huweza kuzaliana
kwa wingi.
“Maeneo
ambayo hayajafuni kwa na maji yanakuwa na nyasi, miti, mizoga na uchafu tofauti
tofauti mbao hutumika kama chakula kwa samaki na vingine vikioza hutoa
vimelea ambavyo vinatumika na mime iliyopo ndani ya maji kutengeneza
chakula pamoja na oxgen” alisema Mwichande.
Akizungumzia
upatikanaji wa sumu zinazotokana na shughuli za kibinadamu ambazo kutokana na
ongezeko la maji alisema hakuna dawa ya kutibu samaki waliopo ziwani kwani
madawa yanayoingia ziwani hubadiilika na kuwa chakula kwa baadhi ya viumbe
walioko majini na hivyo kutoleta mdhara yoyote.
Alisema
kuwa kutokana na muingiliano wa maji kutoka vyanzo tofauti tofauti
vinavyofanya sumu inayosambazwa mpaka inafika ziwani inakuwa haina nguvu tena
kama ambavyo ingaingia bila kukumbanan a vyanzo vingine vya maji.
Akifafanua namna ambavyo
samaki na viumbe wengine wa majini wanavyoweza kupata madhara kutokana na
kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kufuatia ongezeko la maji alisema,
viumbe wanaopatikana katika ziwa, mito, au hata bahari, huishi kwenye maeneo
ambayo temperature, pressure, chemical, light, food na oxgen vinaendana na
viumbe husika.
Mwichande alisema hali hiyo ikitokea
kiumbe akaingia katika maeneo ambayo hajayazoea hujitahidi kurithi mazingira na
akishindwa basi hutafuta namna ya kurudi alipotoka.
Kwa
upande wa mamlaka ya hali ya hewa, Meneja wa kituo Kikuu cha utabiri Mamlaka ya
hali ya hewa Tanzania Samweli Mbuya, alisema wamekuwa wakitoa
utabiri wa hali halisi ilivyo ikiwemo mvua, joto na upepo, na tabiri hizi
zimekuwa zikiambatana na tahadhari hasa mifumo ya utabiri inapoimarika na
kudsababisha mvua nyingi.
Alisema
mvua zinaweza kuwa za muda mfupi au za muda mrefu (za msimu) kwa maana mvua
kuwa juu ya kiwango cha kawaida taarifa zimekua zikitolewa kwa uhakika na
usahihi kabisa.
Akizungumzia
changamoto hiyo wananchi, Rashid Omary alisema wamepata hasara za kichumi
kutokana na soko kujaa maji hali mabayo inakwamisha shughuli za
kibiashara kufanyika vizur.
Pamoja
na kukwama kwa shughuli za kiuchumi, miundombinu ya barabara imethirika ambapo
daraja la linalounganisha kata ya Gungu na Kibirizi lipo katika hatari ya
kubomoka na ubomokaji wake utaleta chanagmoto za usafirishaji.
Muhandisi kutoka NEMC na kaimu mwenyekiti wa bodi ya bonde la ziwa Tanganyika
Delfrina Igulu, amezishauri mamlaka na wanachi kufanya shughuli za
kijamii mita 60 kutoka kwenye vyanzo vyote vya maji na kuseam
kuwa jamii zilizopo pembezoni mwa vyazno vya maji zichukue hatua stahiki
kwaajili ya usala wake.
Benjamini
Dotto Meneja NEMC kanda ya magharibi alitoa wito kwa wawekezaji kufanya
tathmini za athari za mazingira lengo kupata ushauri kutoka kwa wataalamu
mbalimbali kabla ya kuchukua hatua yoyote ya ujenzi kwani mchakato wa
tathmini ya athari utasaidia kupunguza changamoto za kimazingira na za kijamii
kwa uwekezaji endelevu.
“Wananchi
tutekeleze matakwa ya kisheria ya usimamizi wa maji namba 11 ya mwaka 2009
inayotutaka tujenge au tufanye shughuli zetu nje ya mita 60”.
Mwisho.
0 Comments