DHANA YA KUONGEZA UMRI WA KUISHA BAADA YA KUCHOMA MISITU YAHATARISHA MAZINGIRA KIBONDO

 


Na. Adela Madyane, Kigoma.

Wananchi wilayani Kibondo mkoani Kigoma wameshauriwa kulinda mazingira na kuachana na dhana kwamba kuchoma moto misitu huongeza umri wa kuishi.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Misitu na Uhifadhi wa Mazingira wilaya ya Kibondo Bw. Bareth  Ng’umbi wakati akizungumzia suala la uchomaji misitu bila kujali elimu inayotolewa.

Alifafanua kuwa, misitu na uoto wa asili hulinda vyanzo vya maji utokanao na uharibifu wa mazingira, ili kuondokana na uhaba wa maji na upatikanaji wa maji salama na safi, ni lazima wananchi waache tabia ya kuchoma misitu kwa maandalizi ya kilimo na kwa nia nyingine yoyote.

Alisema wilaya ya Kibondo ni miongoni mwa wilaya zilizo na uhaba wa maji, serikali inajaribu kila namna kuondokana na changamoto hiyo kwa kuboresha miundombinu ya maji, lakini wananchi badala ya kupanda miti, wanaharibu uoto wa asili ambao wanategemea.

"Wananchi wanaona jinsi ilivyo ngumu kupata maji safi na salama ndani ya maeneo yao, ni mashuhuda wazuri kwamba vyanzo vya mito vinakauka, mazingira yote ni kavu na tupu, lakini wanaendelea kuchoma misitu, hivi karibuni tutakabiliwa na ukame na kuiacha miundombinu bila maji ”Aliongeza.

Annajesta Paschal mkazi kutoka Kibondo aliwashauri maafisa ugani wa wilaya kuimarisha utoaji wa elimu ya uhifadhi wa misitu na mazingira kwa wananchi bila kuchoka.

Alisema hatua zinazofaa zinapaswa kuchukuliwa kwa wananchi ambao kwa makusudi wanachoma moto na kuharibu mazingira  kama sheria ya mazingira inavyosema.

Kwa upande wake, Matokeo Justine alisisitiza kwamba maafisa ugani hawapaswi kukaa ofisini, wanapaswa kuzungukia jamii na kutoa elimu juu ya athari za kuchoma misitu kwa mazingira kwani kwa sasa wakulima wanaandaa mashamba bondeni, na wanachofanya ni kuchoma moto  nyasi na vichaka ili kurahisha kilimo.

Post a Comment

0 Comments