MAKAMU WA RAIS AITAKA IDARA YA UHAMIAJI KUTOWASUMBUA RAIA WA KIGOMA

 


Na Diana Rubanguka, Kigoma.


Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philipo Mpango, ameiagiza idara ya uhamiaji Mkoa wa kigoma kufanya kazi kwa weledi wanapofuatilia wahamiaji haramu wanaoingia nchini bila kufata taratibu na sheria za nchi.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Kigoma katika Viwanja vya Mwanga Community Centre mkoani hapo akiwa katika wizara yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa makamu wa Rais wa Tanzania.

Aidha Dkt Mpango aliitaka idala ya uhamiaji kuwa ifanye kazi kwa umakini wakati wa kuwatambua wananchi wanaishi mkoa wa Kigoma ambao siyo raia wa Tanzania badala ya  kuwabambikizia kesi ya uhamiaji wananchi wa kigoma ambao ni wazawa na raia wa Kigoma. 

Kufuatia hali hiyo, amewaagiza kukaa pamoja na wabunge ili kujadili namna bora ya kuhakikisha wale ambao  si raia  na wanaishi nchini kinyume na taratibu za nchi wanachukuliwa hatua stahiki na si kumsumbua kila  mwananchi kwa kigezo cha kuzaliwa Kigoma.

“kigoma nzima tumegeuzwa wahamiaji, Mimi mwenyewe nilishabatizwa jina mitandaoni naitwa mrundi na wakati Burundi nimefika mara moja nilipoagizwa na raisi wetu kwenye kumbukizi ya aliyekuwa raisi wa Burundi hayati Nkurunzinza, tusihukumiwe kwakuwa tunaishi Kigoma na tupo karibu na Mipakani" alisema Mpango

“Kumekuwa na kasumba ya kuwakamata na kuwaweka ndani wananchi wa mkoa wa Kigoma kwa kuwabambikizia kesi za uhamiaji hali inayowafanya wanachi kuishi bila amani katika mkoa na nchi wanayozaliwa na kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kiutafutaji kwa kuhofia kukamatwa| aliongeza Dr Mpango.

Katika ziara hiyo amezindua jengo la ofisi za takwimu mkoa wa kigoma ambao amesema kuwa  sensa inayotarajia kufanyika 2022 ni kwa manufaa ya jamii na kusema kuwa  kujua idadi ya watu itasaidia katika kupanga miradi ya maendeleo na kuitambua mahitaji yao kwaajili ya utekelezaji wa huduma wanazostahili.

Hata hivyo kufuatia wimbi la mgonjwa wa Uviko (Covid 19) Dkt Mpango ametoa wito kwa jamii kuendelea kufuata taratibu za kujikinga zinazotolewa na wataalamu wa afya kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo.

“korona ipo, niwaombe ndugu zangu tusifanya mzaha na ugonjwa huu kwani upo na unaua, tuendelee kunawa mikono kwa maji tililika kama tulivyoelekezwa, kuvaa barakoa na kuchukua tahadhari nyingine" alieleza Dkt Mpango 

Akitoa takwimu za ugonjwa huo amesema, mpaka sasa tuna wagonjwa 18 katika mkoa wa Kigoma huku Tanzania nzima wagonjwa wakiwa 471,  kwa takwimu hizi mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa 10 yenye wagonjwa wengi.

 

Post a Comment

0 Comments