WAKULIMA WILAYANI KIBONDO WALIA NA MAAFISA UGANI





Na Mwandishi Wetu, Kibondo

Baadhi ya wakulima wilayani Kibondo mkoani kigoma wameiomba serikali kusisitiza uwajibikaji kwa maafisa ugani kuwatembelea wakulima na kuwapa elimu juu ya magonjwa yanayoshambulia mazao yao ili kulima kilimo chenye Tija na chenye kuleta maendeleo kwa wakulima.

Wakizungumza kwa nyakati Tofauti na blog hii walisema wamekuwa wakitumia Mbinu za kienyeji kutambua magonjwa yanayoshambulia mazao yao , na kwamba  wakati mwingine mazao yamekuwa yakiharibiwa na wadudu kutokana na wakulima kukosa elimu ya kilimo.

Afsa Ugani wilaya ya Kibondo Albert Fatakanwa alisema changamoto inayoikabili wilaya ya hiyo ni uhaba wa maafisa Ugani kulinganishwa na kata za wilaya hiyo , na kwamba wamekuwa wakitumia baadhi ya wakulima viongozi kwenye vijiji kuwaelimisha wakulima wenzao ili kukabilina na changamoto hiyo.

 


Post a Comment

0 Comments