WATOTO 72 WAFANYIWA UKATILI WA KIJINSIA KIGOMA

 


Na Mwajabu Hoza , Kigoma

TAKRIBANI asilimia 72 ya watoto wa kike wamefanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwemo ukatili wa wa kihisia, kimwili na kingono na asilimia 71 ya watoto wa kiume nao wakiwa wamepitia ukatili kama huo kwa mkoa wa Kigoma.

Katika takwimu hizo asilimia 60 ya watoto wamefanyiwa ukatili wa kihisia ikiwemo kutukanwa, kudhalilishwa kwa maneno mabaya na kutishwa na ukatili ambao umeanza kupatiwa Baraka katika jamii na kuonekana ni jambo la kawaida.

Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa mkoa wa Kigoma katika kipindi cha  mwaka 2011  watoto wa kike wamekuwa waadhirika wa matukio ya ukatili ambapo kati ya watoto wa kike 100 wenye umri chini ya miaka 18 asilimia 30 wamefanyiwa vitendo vya ukatili huku kati ya watoto saba wenye umri chini ya miaka saba mmoja kati yao amefanyiwa ukatili.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Murufiti wilaya ya Kasulu Mji mkuu wa Mkoa Kamishna wa polisi Thobias Andengenye amesema matukio hayo yamekuwa yakifanywa na watu wa karibu ikiwemo wajomba, baba, baba wadogo, shangazi, na majirani na ukatili umemgusa kila mtu hivyo jamii inatakiwa kushikamana kwa pamoja kupinga vitendo hivyo.

“Mtoto akibakwa anaweza kutibiwa michubuko lakini maumivu yaliyopo ndani ya moyo hayawezi kutibiwa na daktari na hivyo tunatengeneza watoto ambao wataishi na maumivu miaka yote ya maisha yao.”

Amesema hatuwezi kuwa na jamii ambayo kila mtoto amefanyiwa ukatili hali ambayo inahatarisha usalama wa Taifa kwa kuendelea kutengeneza watoto ambao watakuwa wakiishi na visasi ndani ya mioyo yao hivyo ni vyema wazazi kujenga tabia ya kuzungumza nao , kuwalinda na kuwadhamini watoto kwa kujua changamoto zao na kuzipatia ufumbuzi.

Aidha ameonya tabia ya baadhi ya jamii wakuozesha watoto wao wakiwa katika umri mdogo lakini pia kuacha tabia ya kuwatumikisha watotokatika shughuli za uzalishaji mali na kuwafanya kitegauchumi cha familia na kuhatarisha usalama wa maisha yao mzazi anajukumu la kumpatia mtoto wake elimu bora na malezi mazuri.  

Merania Samweli ni mzazi ambaye ameeleza kuwa ukatili unaofanywa na wanaume kwa wakezao ikiwemo vipigo mara kadhaa umekuwa ukiadhiri malezi ya watoto ndani ya familia na hhivyo kusababisha watoto kukosa malezi bora kutoka kwa wazazi wao.

Post a Comment

0 Comments