Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kasper Mmuya |
Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kasper Mmuya ameitaka jamii kuacha tabia ya kumaliza kesi za ukatili kienyeji na kubainisha kuwa mila na desturi kandamizi zinachangia matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Mmuya amesema mashirika, wadau na taasisi zisizo za kiserikali zishirikiane na Serikali katika kuondoa mila na desturi Kandamizi ambazo zinachangia matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii
Ameyasema hayo leo kwenye
ziara yake mkoani Shinyanga wakati alipo itembelea shule ya Agape inayomilikiwa
na shirika la Agape mkoani humo linalotetea haki za wanawake na watoto
Aidha katika ziara yake amekutana na kamati ya ulinzi na usalama na wanawake na watoto mkoa wa Shinyanga pamoja na wadau wanaotekeleza Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA)
Mmuya ameiomba jamii kuacha tabia ya kumaliza kesi za ukatili kienyeji huku akivishauri vyombo vya dola ikiwemo Polisi na Mahakama kukaa na kujadili namna ya kuondoa changamoto ya ucheleweshaji wa kesi za matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
“Mila
na desturi kandamizi katika maeneo mengi ndiyo inachangia matukio ya ukatili
dhidi ya wanawake na watoto. Mila hizi tunaziendekeza sisi kwa kufanya vikao
ngazi ya familia na kumaliza kesi za ukatili kienyeji. Tunalipana fedha na mali
na kumaliza kesi za matukio badala ya kupeleka kesi kwenye vyombo vya sheria
huku vyombo vya sheria navyo vikilaumiwa kuchelewesha maamuzi matokeo yake
ushahidi unapotea na matukio yanaendelea kutokea”,amesema Mmuya
0 Comments