Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa Serikali Ndg. Gerson Msigwa |
Na Mwandishi Wetu, Singida
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na
msemaji mkuu wa Serikali Ndg. Gerson Msigwa amesema Serikali imeanza
kujenga mahusiano endelevu na waandishi wa habari na taasisi zinazotumia
waandishi wa habari nchini, hatua ambayo inalenga kuhakikisha wananchi wanapata
taarifa sahihi.
Msigwa ameyasema hayo aliookutana na
Rais wa muungano wa klabu za waandishi wa habari nchini UTPC Deogratius
Nsokolo mjini Singida.
Msigwa amesema Serikali inatambua mchango wa
waandishi wa habari na Press Club nchini katika kusimamia maadili na kusaidia
maendeleo katika mikoa mbalimbali na ndio maana ameamua kuweka utaratibu wa
kutoa taarifa za Serikali Kwa kukutana na waandishi katika mikoa mbalimbali.
Amesema hatua hiyo inawapa fursa waandishi
kuuliza juu ya mkoa wao na Taifa.
"Nimemualika Rais wa UTPC hapa Singida
ili kuonyesha azma ya serikali kuwathamini na kuwatumia wandishi wa habari
katika mikoa yote kueleza masuala mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali lakini
Serikali kupata mrejesho kupitia kwao Kwa kuwa ndio wapo karibu zaidi na
wananchi" alisema Msigwa.
Mkurugenzi wa idara ya habari Maelezo na msemaji mkuu wa Serikali Ndg. Gerson Msigwa (wa kwanza kushoto) akiwa na Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Nchini (UTPC) Deogratius Nsokolo baada ya mazungumzo mjini Singida.
Kwa upande wake Rais wa muungano wa klabu za
waandishi wa habari Tanzania Deogratius Nsokolo alimshukuru Msemaji mkuu wa
Serikali Kwa kutambua mchango wa UTPC na Press Clubs nchini pamoja na taasisi
nyingine za habari nchini katika maendeleo ya nchi.
Alisema Press Clubs na UTPC zipo tayari kutoa
ushirikiano wa dhati ili kuhakikisha wananchi habari ambazo zitawasaidia kupata
maendeleo.
Nsokolo pia alimuomba Msemaji mkuu wa Serikali
ambaye pia ni Mkurugenzi mkuu wa idara ya habari Maelezo kushughulikia
changamoto zinazowakabili wanahabari nchini na hasa sheria, mikataba ya ajira
na ujira, mambo ambayo ameahidi kiyashughulikia kupitia bodi ya ithibati
itakayoundwa hivi karibuni.
Aidha Nsokolo amempongeza Msigwa Kwa ubunifu
mbalimbali tangu ateuliwe kushika nyadhifa hizo, ubunifu ambao umefanya
wananchi kupata taarifa za Serikali Kwa urahisi na waandishi kupata taarifa
mbalimbali kupitia mikutano inayofanyika kila jumapili ya wiki.
Msemaji mkuu wa Serikali katika mkutano wake
na waandishi wa habari pamoja na mambo mengine ametoa taarifa kuhusu maendeleo
ya utoaji chanjo ya Uviko 19 na kuwataka wananchi kujitokeza kuchanja ili
kujikinga na ugonjwa huo hatari.
0 Comments